AN-NUUR 
Na.170 Jamadul Akhir 1419, Oktoba 9 - 15, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
 
Msiwageuze watoto ombaomba 
Na H.E. Omar

KWA kipindi cha kama miezi miwili iliyopita karibu kila siku nikipita maeneo ya katikati ya Jiji, Kariakoo na vitongoji vingine maarufu hapa Jijini nakutana na vijana wadogo wanaomba michango kwa watu mbalimbali wanaopita njia hasa wale wanaowahisi ni Waislamu. 

Juzi baada ya kukutana na kijana mmoja ambaye nilishakutana naye siku za nyuma nikaamua kumhoji mara baada ya kuniomba mchango. Mazungumzo yetu yalikuwa hivi: 

Mtoto: Dada Assalaam Alaykum. Shikamoo naomba mchango wa madrasa. 

Baada ya kuitikia salamu yake niliendelea kumhoji. 

Swali: Umejuaje kama mimi Muislamu? 

Jibu: Umevaa baibui na ushungi hivyo bila shaka ni Muislamu. 

Swali: Mimi nitafahamu vipi kama wewe kweli ni Muislamu na huo mchango ni wa madrasa? 

Jibu: Mimi ni Muislamu haki ya Mungu vile. Huoni nimevaa barakashia, jina langu hili hapa (aoanyesha jina kwenye fomu ya michango aliyokuwa nayo). 

Swali: Chuo chenu kiko wapi? 

Jibu: Temeke kwa (nimesahau jina alilolitaja). 

Swali: Saa hizi saa tatu asubuhi wewe skuli unaenda saa ngapi na mchango unakusanya saa ngapi na wakati huo huo chuo unasoma saa ngapi? 

Jibu: Nimeshamaliza darasa la saba. Chuoni tunaenda jioni. 

Swali: Si juzi tu tumekutana Posta ya Zamani ukaniambia upo la tano hivyo unaingia jioni skuli? Au sio? Leo umeshamaliza? 

Jibu: Sio mimi kweli tena labda umenifananisha tupo wengi Wallah vile. 

Swali: Kwanini walimu wenu hawachangishi hiyo michango wenyewe? 

Jibu: Hata wao wanachangisha lakini sisi ndo tunakuja mjini kwa sababu nauli yetu "fisi" tu (50) na tunapata pesa kibao. 

Swali: Unafikiri kwa nini nyie mnapata pesa nyingi kuliko walimu wenu? 

Jibu: Tunatembea sana, watu wanatuonea huruma hivyo watugea pesa japo jiti tu (100) siku za Ijumaa kwa Wahindi unapata pesa kibao. 

Swali: Mmeanza lini kuchangisha pesa hizo na mnadhani mtapata kiasi gani pia mnategemea kumaliza lini? 

Jibu: Tumeanza siku hizi hizi, hata sijui tutamaliza lini, tukimaliza Ustaadh huwa anatuambia hayatuhusu sisi tuchangishe tu. 

Swali: Wazazi wako wanafahamu kama unafanya zoezi hili la uchangishaji? 

Jibu: Mwalimu wa chuo mwenyewe babangu mdogo. Dada wewe Paparrazi nini. Mbona maswali mengi? 

Swali: Nikikwambia siwezi kukupa pesa zangu kwani mimi siamini kama hizi pesa kweli walimu wenu wanazitumia kuendeleza madrasa utasemaje? 

Jibu: Siwezi kukulazimisha, pesa si yako! Wewe si Muislamu ("ndio") na mimi si Muislamu bassi haiwi kwa watu wawili Waislamu kuacha kuaminiana. Toa tu dada utaikuta amali yako kwa Mwenyezi Mungu. 

Swali: Hivi unadhani watu watawatafautishaje na ombaomba? 

Jibu: Mimi sio kilema, wala sio kipofu, na ninakaa kwetu pia ninayo fomu hii hapa ya kujaza ambayo ombaomba hawana. (Mwisho. Sikuwa na Cassette wala sikuandika hivyo nimenukuu kwa kadri Allah (sw) alivyonijalia kukumbuka). 

Kwa kumuonea huruma ya kumpotezea muda wake nikampa kiasi cha pesa na kumruhusu aondoke. 

Ndugu zangu katika Uislamu hawa watoto ambao wanalelewa katika mazingira haya tunategemea baadaye waje kuwa kitu gani? 

Nyie walimu wa chuo (madrasa) hamuoni mnaudhalilsha, ufedhehesha na kuudunisha Uislamu na Waislamu. 

Hawa watoto walivyo tu huzuni tosha kabla hawaja nyanyua mdomo kuomba mchango. Sijui mtu anayesoma Madrasa Temeke anafikaje Posta akiwa pekupeku. Ni wachafu na kwa haraka haraka unaweza kudhani ni vibaka fulani. 

Hivi kuna uhusiano gani kati ya uchafu au kuwa rough na Uislamu. Au Waislamu wanatakiwa uwa wasafi siku ya Ijumaa an siku za Eid? 

Wazazi mnaowapeleka watoto wenu madrasa ili wakafundishwe kuwa ombaomba si bora muwafundishe wenyewe japo mara mbili kwa wiki au dufu ni kitu muhimu sana hivyo ni lazima watoto waende madrasa. 

Hivi mzazi unaweza kumuachia mwanao aende skuli peku, hajachana nywele na akiwa uniform chafu? Mbona chuoni vitu hivi hamvijali? 

Waislamu tuache kujidhalilisha, Uislamu ni dini ya usafi sio dini ya kanzu zenye viraka. Tusikubali kudhalilishwa kwa kuhakikisha tunapiga vita juhudi zozote zile za Uislamu hasa kwa walimu wa madrasa wanaowageuza watoto (Waislamu) kuwa ombaomba. Kwa mtaji huu hatutafika popote. 

"Ee Allah tujaalie tuweze kuurejesha Uislamu katika nafasi yake hapa duniani" 
 

 
Juu 
 

YALIYOMO 
 
 

TAHARIRI 
Tutaendelea kudhalilishwa mpaka lini ? 

Waislamu wasisitiza: Nyumba ya Waziri Mkuu ni ya Waislamu 
Na Mwandishi Wetu 

Kuchomwa nyumba za wananchi 
Na Mwandishi wetu 

Maoni Yetu: 
Maisha ya Mtanzania yanapokosa thamani 

Nguruwe marufuku Kinondoni – Tume 
Na Kassim Juma 

Watanzania waanzisha Baraza la Waislamu Marekani 
Na Mwandishi Wetu 

Wanawake Hai wamtaka Rais azungumzie mauaji ya Mwembechai 
Na Mwandishi Wetu 

‘Serikali haiwezi kuzuia rushwa’ 
Na Kassim Msuya 

Makala ya Kimataifa 
Nani gaidi: Slobodan Milosovic au Usama bin Laden 
Na Mwandishi Wetu 

Afghanistan washindi dhidi ya uvamizi karne zote 
Na Faiza bint Abubaka 

MAKALA: 
Demokrasia ya rushwa ! 
Na Mwapwani Mohamed 

Tujikwamue na janga la utwaghuti 
Na I. Kikong’ona 

MAONI: 
Nini Jihad na nani Mujahidina ? 

MAKALA: 
Marekani ni magaidi wa haki za binadamu 
Na MUSSA ALLY 

Tufuate Uislamu kwa vitendo na siyo kwa maneno -2 
Mwandishi: Maalim Ali Bassaleh 

Tusihalalishe mauaji ya raia kwa kisingizio cha ‘wananchi wenye hasira’ 
Na Mwandishi Wetu 

Historia ya sayansi na tiba 
Na Dk. Amur A.A. 

Msiwageuze watoto ombaomba 
Na H.E. Omar 

MAKALA YA JAMII: 
Profesa Malise Kaisi acha uzushi dhidi ya Mtume Muhammad 

Sensa ya majaribio: Wananchi watofautiana na serikali 
Na Rajab Rajab - Morogoro 

Uislamu ulivyoingia Zanzibar -3 

Mwembechai wageuka Hame, Bado walindwa na polisi 
Na Badru Kimwaga 

Waislamu Moro waendelea kusaidia wagonjwa 
Na Rajab Rajab - Morogoro 

Mjadala wa Katiba ya Shirikisho kuzinduliwa Dar Jumapili 
Na Mohamed Othman 

Walimu wa dini Tanga wapokea Baiskeli 
Na Abu Said 

Mafundisho ya Quran 
Kutoa katika njia ya Allah: Al-Baqarah aya  264 

Barua za wasomaji 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Chakula na Lishe 
Vitu vinavyoweza kuwemo katika vyakula 

 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtz.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita