|
|
| Sensa
ya majaribio
Wananchi watofautiana na serikali Wadai ufujaji fedha umekithiri BAADHI ya wananchi mjini hapa wameonyesha kutoridhishwa kwao na maamuzi ya Serikali kufanya sensa ya majaribio na kudai kuwa huo ni ufujaji wa fedha unaofanywa na serikali kwa lengo la kuwanufaisha wachache. Wakiongea na gazeti hili kwa nyakati tofauti mapema wiki hii wananchi hao wanawake kwa wanaume wamedai kuwa kama ni majaribio tayari serikali iimekwisha kufanya na kupata uzoefu tangu sensa ya 1978 na 1988, hivyo majaribio hayo hayakustahili kuwapo bali ilitakiwa kutekeleza sensa ya kila baada ya miaka kumi kama ilivyojiwekea. "Hatudhani kama serikali yetu imefanya vyema kufanya sensa inayoiita ya majaribio ambayo imetumia mamilioni ya fedha huku wananchi wake wakikosa huduma muhimu kwa kisingizio serikali haina fedha", alisema Bi. Christina Mwaipopo aliyejitambulisha ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine Morogoro. Naye Bw. Mussa Salum Mkeri wa Kiwanja cha Ndege mjini hapa amedai kuwa serikali ina agenda ya siri kuhusu sensa ya majaribio kwani hakuna mantiki yoyote kufanya sensa hiyo wakati sensa kuu ni mwakani. Alisema Bw. huyo bila kufafanua. Akitoa mchango wake juu ya sensa hiyo Bw. Hashim Hamza ambaye ni mwanafunzi wa masomo ya uchumi mwaka wa pili IDM - Mzumbe amesema kuwa serikali haikuwa na sababu yoyote ya msingi kuweka sensa hiyo ya majaribio. "Sioni kama kulikuwa na ulazima wowote wa kufanyika sensa hiyo, wakati tunatarajia kufanya sensa ya jumla sasa hii hali inachangia kudumaza uchumi wetu kutokana na fedha kutumika ovyo", alisema mwanafunzi huyo. Akieleza malengo ya sensa hiyo wakati akiongea na vyombo vya habari hivi karibuni Kamishna wa Sensa hiyo Dk. Damas Mbogoro amesema wanafanya hivyo ili kupata uzoefu wa mazingira hususan mabarabara kutokana na nyingi kuharibiwa na mvua, pamoja na kuangalia maeneo yenye msongamano mkubwa wa watu. Sensa hiyo ya wiki moja inafanyika katika miji ya Iringa, Bagamoyo, Wilaya ya Makete, Wilaya ya Kahama na Kusini Pemba katika Wilaya ya Chache Chake. Sensa hiyo itagharimu zaidi ya shilingi milioni 60 ikiwa ni posho kwa maofisa wa sensa wapatao 238 pamoja na vifaa vingine vinavyohitajika katika sensa hiyo. Sensa ya Kitaifa inatarajiwa kufanyika Agosti 29,1999 baada ya kushindikana
kufanyika mwaka 1997 kufuatia mvua kubwa zilizonyesha kwa kipindi kirefu.
|
YALIYOMO
TAHARIRI Tutaendelea kudhalilishwa mpaka lini ? Waislamu wasisitiza: Nyumba ya Waziri
Mkuu ni ya Waislamu
Kuchomwa nyumba za wananchi
Maoni Yetu:
Nguruwe marufuku Kinondoni – Tume
Watanzania waanzisha Baraza la Waislamu
Marekani
Wanawake Hai wamtaka Rais azungumzie
mauaji ya Mwembechai
‘Serikali haiwezi kuzuia rushwa’
Makala ya Kimataifa
Afghanistan washindi dhidi
ya uvamizi karne zote
MAKALA:
Tujikwamue na janga la utwaghuti
MAONI:
MAKALA:
Tufuate Uislamu kwa vitendo
na siyo kwa maneno -2
Tusihalalishe mauaji ya
raia kwa kisingizio cha ‘wananchi wenye hasira’
Historia ya sayansi na tiba
Msiwageuze watoto ombaomba
MAKALA YA JAMII:
Sensa ya majaribio: Wananchi watofautiana
na serikali
Uislamu ulivyoingia Zanzibar -3 Mwembechai wageuka Hame,
Bado walindwa na polisi
Waislamu Moro waendelea kusaidia
wagonjwa
Mjadala wa Katiba ya Shirikisho
kuzinduliwa Dar Jumapili
Walimu wa dini Tanga wapokea
Baiskeli
Mafundisho ya Quran
Chakula na Lishe
|