AN-NUUR 
Na.170 Jamadul Akhir 1419, Oktoba 9 - 15, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
 
Nguruwe marufuku Kinondoni – Tume

Na Kassim Juma 

TUME ya Jiji Kanda ya Kinondoni imetoa amri ya kusimamisha uuzaji wa nyama ya nguruwe katika maeneo mchanganyiko. 

Amri hiyo ya Tume imo katika barua yake ya Septemba 29, 1998 iliyosainiwa na Bw. E. B. Paul kwenda kwa mmiliki wa bucha moja iliyopo Hananasif Mkunguni Kinondoni. 

Aidha, barua hiyo imemtaka mmiliki huyo kumuona Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo kwa ajili ya kile ilichokieleza kuwa kupata maelezo na ufafanuzi zaidi. 

Amri ya Tume ya Jiji imefuatia malalamiko ya wananchi wa kata ya Kinondoni dhidi ya mmiliki wa Pork Butcher nyumba Na. AN 381. 

Hata hivyo, imedaiwa kuwa licha ya kuwepo amri hiyo ya Tume ya Jiji, hadi kufikia Oktoba 6, 1998 mmiliki huyo alikuwa bado akiendelea na biashara hiyo. 

Baadhi ya wananchi waliofika katika ofisi ya gazeti hili wameahidi kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa amri hiyo. 

Wamesema wametoa muda kwa Tume ya Jiji kuhakikisha amri hiyo inatekelezwa, vinginevyo wametishia kuchukua hatua mikononi. 

Uuzaji na ufugaji wa nguruwe holela umeibua malalamiko sehemu mbalimbali Jijini. 

Hata hivyo, malalamiko hayo yamekuwa yakikumbana na maelezo ya jumla jumla au kimya kizito kutoka kwa wahusika. 
 
Juu 
 

YALIYOMO 
 
 

TAHARIRI 
Tutaendelea kudhalilishwa mpaka lini ? 

Waislamu wasisitiza: Nyumba ya Waziri Mkuu ni ya Waislamu 
Na Mwandishi Wetu 

Kuchomwa nyumba za wananchi 
Na Mwandishi wetu 

Maoni Yetu: 
Maisha ya Mtanzania yanapokosa thamani 

Nguruwe marufuku Kinondoni – Tume 
Na Kassim Juma 

Watanzania waanzisha Baraza la Waislamu Marekani 
Na Mwandishi Wetu 

Wanawake Hai wamtaka Rais azungumzie mauaji ya Mwembechai 
Na Mwandishi Wetu 

‘Serikali haiwezi kuzuia rushwa’ 
Na Kassim Msuya 

Makala ya Kimataifa 
Nani gaidi: Slobodan Milosovic au Usama bin Laden 
Na Mwandishi Wetu 

Afghanistan washindi dhidi ya uvamizi karne zote 
Na Faiza bint Abubaka 

MAKALA: 
Demokrasia ya rushwa ! 
Na Mwapwani Mohamed 

Tujikwamue na janga la utwaghuti 
Na I. Kikong’ona 

MAONI: 
Nini Jihad na nani Mujahidina ? 

MAKALA: 
Marekani ni magaidi wa haki za binadamu 
Na MUSSA ALLY 

Tufuate Uislamu kwa vitendo na siyo kwa maneno -2 
Mwandishi: Maalim Ali Bassaleh 

Tusihalalishe mauaji ya raia kwa kisingizio cha ‘wananchi wenye hasira’ 
Na Mwandishi Wetu 

Historia ya sayansi na tiba 
Na Dk. Amur A.A. 

Msiwageuze watoto ombaomba 
Na H.E. Omar 

MAKALA YA JAMII: 
Profesa Malise Kaisi acha uzushi dhidi ya Mtume Muhammad 

Sensa ya majaribio: Wananchi watofautiana na serikali 
Na Rajab Rajab - Morogoro 

Uislamu ulivyoingia Zanzibar -3 

Mwembechai wageuka Hame, Bado walindwa na polisi 
Na Badru Kimwaga 

Waislamu Moro waendelea kusaidia wagonjwa 
Na Rajab Rajab - Morogoro 

Mjadala wa Katiba ya Shirikisho kuzinduliwa Dar Jumapili 
Na Mohamed Othman 

Walimu wa dini Tanga wapokea Baiskeli 
Na Abu Said 

Mafundisho ya Quran 
Kutoa katika njia ya Allah: Al-Baqarah aya  264 

Barua za wasomaji 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Chakula na Lishe 
Vitu vinavyoweza kuwemo katika vyakula 

  

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtz.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita