|
|
|
Wamchangia mama
Chuki sh. 30,000
Na Mwandishi Wetu WANAWAKE wa Kiislamu wilayani Hai mkoa wa Kilimanjaro, wamemtaka Rais atoe kauli na kuunda Tume kuchunguza kwa kina vurugu zilizotokea Mwembechai ambazo zilisababisha kuuawa watu wanne na wengine kadhaa kujeruhiwa. Wanawake hao walitoa kauli hiyo katika kongamano lao lililofanyika siku ya Jumapili Oktoba 4, 1998 kijijini Mudio tarafa ya Masama Mashariki wilayani humo. Kauli ya pamoja ya wanawake hao ilifuatia maelezo ya mtoa mada mmoja katika kongamano hilo aliyeeleza kwa kirefu kadhia ya Mwembechai iliyopelekea polisi kuua raia mwezi Februari mwaka huu. Kwikwi za vilio zilisikika hapa na pale baada ya mtoa mada huyo kukumbusha kuwa pamoja na kuwepo dalili zote zinazoashiria kukiukwa Katiba ya nchi, Rais hajazungumzia chochote hadi hivi sasa. Wanawake hao waliazimia mwishoni mwa kongamano hilo kutorudia makosa ya kuwarejesha madarakani watu wanaowapuuza baada ya kuwachagua. Aidha, walichanga shilingi 30,000 kwa ajili ya pole kwa mama Chuki anaeendelea kumuuguza mwanawe aliyejeruhiwa kwa risasi katika kadhia hiyo. Na Kassim Msuya SHEIKH Abeid wa Msikiti wa Manyema Jijini, amesema katika khotuba ya Ijumaa ya Oktoba 2, mwaka huu kuwa serikali pamoja na taasisi zake haiwezi kuzuia rushwa nchini. Akiwakhutubia waumini waliofurika kuswali sala ya Ijumaa Msikitini hapo, Sheikh Abeid alisema wakati ambapo taasisi za serikali ndizo zingetakiwa kuwa mstari wa mbele katika kupiga vita zenyewe zimekuwa mstari wa mbele katika kupokea, alizitaja baadhi ya taasisi hizo kuwa ni mahakama na polisi. Sheikh Abeid amesema, inachofanya serikali ni kuwadanganya wananchi kuwa inapambana haiwezi wakati watendaji wake ndio wanaoongoza kwa ulaji rushwa. Amesema sababu kubwa zinazopelekea kuongezeka kwa matendo ya upokeaji rushwa ni mifumo ya maisha iliyoundwa na wanaadamu na akaongeza kuwa hakuna chama chochote kitakachoweza kutokomeza rushwa hapa nchini. Akasisitiza kuwa ni Uislamu pekee ndio unaoweza kumaliza tatizo hili kwani Uislamu umeweka namna ya kuzuia kutokea kwa matatizo kama hayo kabla ya hayajatokea. Alitoa mfano kuwa, Mtume (saw) siku moja alimtuma mmoja katika wafuasi wake akakusanye zakat alipo rudi akamkabidhi Mtume fungu moja la zakat na kumwambia Mtume (saw) kuwa hili fungu lingine ni la kwangu. Mtume (saw) akakikema kitendo kile na kumwambia anadhani kuwa angekuwa nyumbani kwake angepata fungu lile? Jibu likawa hapana, kwa hali hiyo Mtume akakilaani kitendo kile na kukifananisha haiwezi. Baada ya kunukuu hadithi hiyo, Sheikh Abeid alisema matendo kama hayo yapo mengi na yamekuwa ndio mtindo wa maisha. Sheikh Abeid aliendelea kusema leo hii nyumba za Wakfu zinageuzwa mabaa akatoa mfano nyumba iliyotolewa Wakfu na Hajat Aziza Omar na kusema kesi ya nyumba hiyo imeendeshwa kwa misingi isiyoeleweka mpaka hukumu ikatolewa bila upande wa Waislamu kujulishwa mpaka baada ya miezi mitatu kupita. Sheikh Abeid alimalizia khotuba yake kwa kuwataka Waislamu kupiga vita rushwa ya namna yoyote ile kwani Uislamu umepinga kila kinachopelekea katika utoaji au upokeaji rushwa. |
YALIYOMO
TAHARIRI
Waislamu wasisitiza: Nyumba ya Waziri
Mkuu ni ya Waislamu
Kuchomwa nyumba za wananchi
Maoni Yetu:
Nguruwe marufuku Kinondoni – Tume
Watanzania waanzisha Baraza la Waislamu
Marekani
Wanawake Hai wamtaka Rais azungumzie
mauaji ya Mwembechai
‘Serikali haiwezi kuzuia rushwa’
Makala ya Kimataifa
Afghanistan washindi dhidi
ya uvamizi karne zote
MAKALA:
Tujikwamue na janga la utwaghuti
MAONI:
MAKALA:
Tufuate Uislamu kwa vitendo
na siyo kwa maneno -2
Tusihalalishe mauaji ya
raia kwa kisingizio cha ‘wananchi wenye hasira’
Historia ya sayansi na tiba
Msiwageuze watoto ombaomba
MAKALA YA JAMII:
Sensa ya majaribio: Wananchi watofautiana
na serikali
Uislamu ulivyoingia Zanzibar -3 Mwembechai wageuka Hame,
Bado walindwa na polisi
Waislamu Moro waendelea kusaidia
wagonjwa
Mjadala wa Katiba ya Shirikisho
kuzinduliwa Dar Jumapili
Walimu wa dini Tanga wapokea
Baiskeli
Mafundisho ya Quran
Chakula na Lishe
|