AN-NUUR 
Na.171 Jamadul Akhir 1419, Oktoba 16 - 22, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
 
Mishikaki ya nguruwe Moshi yachomwa mbele ya Msikiti  

Na Mwandishi Wetu 

NYAMA ya nguruwe imekuwa ikichomwa na kuchemshwa hatua chache kutoka Msikiti wa Suni Mjini Moshi na kuuziwa wapita njia. 

Vibanda viuzavyo nyama hiyo vipo karibu na Ofisi za Mabasi ya Shabaha na imekuwa ni kero kubwa kwa wananchi kutokana na harufu hiyo ya Mishikaki ya nguruwe. Lakini ukaribu wa msikiti kumefanya kero iwe kubwa zaidi. 

AN-NUUR iliwasiliana na Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi, akadai kwamba washapata habari juu ya kero hiyo. 

AN-NUUR pia iliwasiliana na Katibu wa Wilaya wa CCM, Bw. Kibaya ambaye alidai kwamba wao CCM wamewapangisha wafanya biashara lakini hawana mkataba wa kuwapangia wauze nini. 

Mgahawa ambao umekuwa mashuhuri sana kwa uuzaji wa mishikaki hiyo ya nguruwe na zile za kuchemsha unajulikana kwa jina la Kisanga Min-Restaurant - Chekanao - karibu sana na ofisi za mabasi ya Shabaha. 

Wakati huo huo, biashara ya kuuza nyama ya nguruwe mbichi, mishikaki na ile ya supu imekuwa ikishamiri katika maeneo yafuatayo Jijini Dar es Salaam. 

1) Katika barabara ya kutoka Sigara kuelekea Bonde la Msimbazi hadi Vingunguti karibu na nyumba moja ya ghorofa. 

2) Katika barabara ya kutoka Sigara kwenda Chang’ombe (barabara ya kokoto) kwenye njia panda karibu na mti mkubwa. 

3)Karibu na maghorofa ya Kota za Chang’ombe kati ya barabara inayoelekea Kimanga/Kisukuru na inayoelekea Segerea kutoka kituo cha mwisho cha mabasi ya Tabata/Chang’ombe. 

4) Katika Bar moja inayoitwa Angala Bar (Kiti Moto) karibu na Hai Bar iliyoko Tabata. 

5) Karibu na Hotel ya Aroma kwenye njia ya miguu inayoelekea Matumbi Bar karibu na reli (sehemu hii inauzwa kila siku). 

Bisahara hiyo imekuwa ikiongezeka sambamba na ufugaji wanguruwe usiozingatia sheria. 

Katika kikao cha pamoja cha Misikiti ya Liwiti, Tabata, Kimanga, Kisukuru na Segerea, Waislamu wameitaka Serikali ichukue hatua kabla ya wananchi wakereketwa kuchukua hatua wao wenyewe.  

 
Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
TAHARIRI 
Serikali iwahurumie wananchi wake 

KUCHOMWA MOTO NYUMBA ZA WANANCHI: Nzasa wamtaka Mkapa awaonyeshe pa kwenda 
Na Mwandishi Wetu, Nzasa 

Mishikaki ya nguruwe Moshi yachomwa mbele ya Msikiti 
Na Mwandishi Wetu 

MAONI YETU: 
Je; ni halali kuchoma Kidungu cha mtu? 

Upimaji huu mpya ni wa nini 
Na Mwandishi Wetu 

TANGAZO LA HIFADHI YA MSITU WA KAZIMZUMBWI 

Ndoa si lengo, ni wasila wa kufikia lengo 
Na Bi. Zuhura Tajiri, Shinyanga 
 
Teknologia:
Jifunze kuunganisha Kompyuta
Na Hassan Omar

Makala:
Nani atakayewahoji Waheshimiwa hawa

Goda Muslim School, Manzese
Na Mwandishi Wetu

Utabiri sahihi wa kuibuka kwa Uislamu
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa

Historia ya mgogoro wa Nzasa
Na Mwandishi Wetu

DUMT watoa msaada kwa walioathirika Nzasa
Na Mwandishi Wetu

UCHOMAJI NYUMBA NZASA: Wafadhili wana mchango gani?
Na Mwandishi Wetu

Mafundisho ya Quran 
Kutoa pasipo masimango 

Barua za wasomaji 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Chakula na Lishe  

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtz.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita