AN-NUUR 
Na.176 Shaaban  1419, Novemba 20 - 26, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Kondom sio kinga ya Ukimwi

Virusi vya HIV hupenya 
 
 

Wananchi wengi wataendelea kuteketea kwa ukimwi kutokana na dhana potofu waliyo nayo kwamba kondomu ni jawabu katika kuzuia ukimwi. 

Taarifa ya Shirika la Viwango nchini (TBS) iliyotolewa hivi karibuni na kunukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari imewaonya wananchi waepukane na dhana kwamba kondomu zitawanusuru kuambukikizwa ukimwi. 

Kwa mujibu wa Taarifa hiyo iliyonukuliwa na gazeti moja la kila wiki katika toleo lake la Alhamisi Novemba 19; ukimwi umekuwa ukikua kwa kasi kubwa sana hapa nchini ambapo zaidi ya Watanzania milioni moja unusu (milioni 1.5) wamesha ambukizwa virusi hivyo. Kasi hiyo ya kuongezeka kwa ukimwi imekuwa ikienda sambamba na ongezeko la matumizi ya "Salama" kondom na nyinginezo. 

Likinukuu taarifa ya T.B.S. gazeti hilo limesema kwamba, "ni rahisi kwa 

kirusi cha ukimwi kupenya katika kondomu kwa sababu katika darubini za kawaida kondomu zinaonyesha kuwa na matundu ambayo ni makubwa zaidi ya mara 50 ya ukubwa wa kirusi cha ukimwi ambacho hakiwezi kuonekana kwa darubini hiyo hiyo. Mfano wake ni kama mtegemea mchanga usipite kwenye "wiremesh" (waya wa kashata wa dirisha). 

Aidha, taarifa hiyo imeeleza kwamba ukimwi nchini Uganda unapungua kwa wananchi kubadili tabia za uasherati wakati Tanzania kipaumbele kimekuwa katika matumizi ya kondomu. 

Toka kampeni za matumizi ya kondomu kama kinga ya ukimwi zilipoanza gazeti hili limekuwa likiwatahadharisha wananchi kwamba kondomu si kinga ya ukiwmi kwa sababu; kwanza virusi vya HIV ni vidogo sana kiasi kwamba vinaweza kupenya kwenye matundu ya kondomu. Pili, yaweza kupasuka na tatu kuvuja (spillage), 

Aidha, tumekuwa tukisisitiza kwamba upo utapeli unaofanyika katika biashara ya kondomu ambapo wananchi hupewa taarifa za uongo. 

Kwa tamaa ya kuzoa mapesa wafanya biashara wamekuwa wakiwahadaa watu kwamba waweza kumchezea mamba au simba mwenye njaa na wakawa salama ilimradi wana "Salama kondomu" mkononi. Dhana hii ilipotiliwa nguvu na viongozi wa Serikali pamoja na vyombo vya habari soko likazidi kukua. 

Kwa kipindi cha zaidi ya miaka mitano ambapo gazeti hili limekuwa likizungumzia hoja hizi na kuonekana wa 1947; ni roho ngapi zimeteketea kwa kufuata dhana potofu ya uzinzi salama. 

Nani atalipa gharama na fidia ya hasara iliyotokana na kampeni za awali? 

 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
Maoni 
Kuwa na mawazo ya kufugwa tunajidharaulisha 

Sakata la mabucha  ya Nguruwe kuibuka upya 
Na Mwandishi Wetu  

Kondom sio kinga ya Ukimwi 

Bakwata yairushia polisi makombora Ngaramtoni 

MACHO YA SHUTUMA 
Na Abu Halima Sa Changwa 

Serikali yatakiwa iwachukulie hatua wauaji 
Na Mwandishi Wetu 

Historia ya Msikiti wa Ngaramtoni 

Silaha yetu ni kura ya pamoja 
Na Alhaj Yusuf Kalala, Washington DC  U.S.A 

Anuani ya fikra 
Na Abu Halima Sa Changwa 

Kuukaribisha mwezi mtukufu 

Tunahitaji "UN' ya Waislamu! 
Na Said  Rajab 

Kongamano la wanawake wa Kiislamu Newala lafana 

Umuhimu wa Elimu ya Awali kwa watoto wadogo - 2 
Na Ustaadh Kupa Pazi Said 

Kesi mojawapo ya mihadhara yafutwa 

Wasaidieni watoto wenye vipaji - Prof. Kilonzo 

Mahafali ya kidato cha nne Thaqafa: Wazazi wakumbushwa wajibu wao 

Wanafunzi Mwanza wadai haki za kuabudu mashuleni kwa usawa 
Na Iddi M. Katiba, Mwanza 

Saidianeni katika shida - Sheikh Abdallah 

Waislamu, Wakristo Rufiji watakiwa kuunda umoja 

Someni  muiokoe jamii kimaadili 

Acheni Shirki 

Kesi nyingine ya Waislamu Mwembechai yaahirishwa 
Na Muhibu Said 

Kusilimu kwa Wakristo kwaleta kero Mwanza 

Nzasa waomba msaada wa chakula, madawa 

Katibu wa Bakwata Moro ang'olewa Msikitini 

Masomo ya Dini ya Kiislamu  

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Umuhimu wa chakula katika shule za awali] 
 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtz.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita