|
|
| Mafundisho
ya Quran:
Kutoa Sadaka kwa siri -3 Al-Baqarah aya ya 272 Kinachojitokeza katika aya hizi ni kuwa kwanza mtu mwenyewe hufanya uchaguzi wa ama wema au ubaya na ndipo Allah humuwafikisha katika uchaguzi wake huo. Katika aya ya kwanza mbali na Allah kutoa nafasi sawa kwa wanadamu wote ya kuongozwa kwa njia ya ilhamu kwa kueleweshwa mema na maovu, (Na naapa kwa nafsi (roho) na Aliyeitengeneza; kisha akaifahamisha ouvu wake na wema kwake), wanadamu wote wamepata fursa ya kuletewa Mitume ambao wamekuja na vitabu ili kuwafahamisha uongofu pamoja na kuwakumbusha yale ambayo tayari wameshafahamishwa kwa njia ya ilhamu. Iwapo binadamu ameshafahamishwa wema na uovu na akaletewa Mtume akiwa na kitabu kumkumbusha hivyo huyu anaweza kusema kuwa amepotoshwa na Allah? au mtu huyu ana haki ya kusema kuwa Allah hakutaka kumuongoza? Aya ya pili inaelezea uongofu wa Allah na hamna anavyoongoka mtu. Kama ilivyo kwa aya iliyotangulia, Allah anamuwafikisha kuongoka yule ambaye ameletewa uongofu na akaupokea na kisha akaufuata. Na hii ndiyo maana ya kumuongoza yule "aliyeelekea kwake." Ama kwa upande wa nani awe Mtume na nani asiwe hilo Allah hulifanya mwenyewe hata kabla ya mtu anayehusika kuzaliwa. Mitume wote huzaliwa Mitume ingawaje wenyewe hawajifahamu hadi wanapodhihirishiwa na Allah wakati unapofika. Mitume wengi pamoja na kuwa na sifa tofauti na watu wa jamii zao walijifahamu kuwa wao ni Mitume walipotimia miaka 40 na kutangaziwa hivyo na Allah Mwenyewe au Malaika Jabril (a.s.) Kwa kuwa aya tunayoendelea nayo (272) imo katika mtiririko wa kutoa inakamilika kwa kuelezea mambo mawili ya msingi: -mtu anapotoa mali yake huwa ni kwa manufaa yake binafsi na siyo anapoteza bali atarudishiwa kwa malipo yaliyo bora zaidi kuliko hicho kidogo alichokitoa. - Mtu anapotoa anatakiwa afanye hivyo kwa lengo moja tu ambalo ni kumridhisha
Allah Ambaye ndiye aliyetoa agizo hilo. Kutoa kwa matarajio mengine yasiyo
ya kupata radhi za Allah kutampelekea mtoaji kuwemo hasarani.
|
YALIYOMO
Maoni Waislamu tunakusudiwa kufanywa watumwa wa nani? Wananchi waingiwa na hofu kuhusu silaha Serikali yagwaya kwa wafugaji
nguruwe
Hakuna njama za kupindua Bakwata - Sheikh Yahya MARADHI YA KISAIKOLOJIA:: VOYEURISM
Tathmini: Miaka 37 ya uhuru wa Tanganyika
Mdahalo kati ya Waislamu na Wakristo:
Batendi hakumuelewa Mkomidachi
Muhammad (s.a.w.) katika
Unabii wa Isaya (a.s.)
Ijue SUA Madrasa Moro
Kiteto wakosa darsa kwa kupinga Ramli Ustadh ayeyuka na saruji ya Msikiti mjini Arusha Akina mama Muheza waungana kufanya
Daawa
Wanafunzi Waislamu Mbeya wapata
uongozi
Je, hivi tuendelee kushika amri
za Mungu tena? - 2
Njia ya uzima ni nyembamba,
waionao ni wachache - 2
Waandishi andikeni ukweli - Kamati
Sheikh Jongo aichachamalia
Uwawaru
Waamriwa kurejesha Mali ya
Mirathi
Waislamu Mlimba Moro mashakani
Sayansi na Teknolojia
Chakula na lishe
|