AN-NUUR 
Na.180 Shaaban 28 - Ramadhan 1419, Desemba 18 - 24, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
UWAWARU yafa Rufiji 
 
  • Masheikh wasutwa Msikitini
  • Waangua vilio kwa huzuni
UMOJA wa Waislamu na Wakristo Rufiji (UWAWARU) umeripotiwa kusambaratika baada ya upande wa Waislamu ukiongozwa na Sheikh Shaharani kujitoa. 

Taarifa kutoka Rufiji zinaeleza kwamba kujitoa kwa Waislamu kulifuatia mkutano wa pamoja wa Waislamu wa Ikwiriri uliofanyika Msikitini mwanzoni mwa wiki hii. 

Awali, mkutano huo ilikuwa ifanyike siku ya Ijumaa Desemba 11, mwaka huu hata hivyo uliahirishwa kutokana na wahusika wakuu kutohudhuria. 

Kwa mujibu wa waliohudhuria kikao hicho, muumini mmoja ambaye alifahamika kuwa ni muhudumu wa Msikiti huo huku akititirikwa na machozi alimkabili Sheikh wa wilaya wa Bakwata Kassim Rwambo na kumwambia kwamba hali ya kukosa kujifahamu kwa baadhi ya waumini imesababishwa na yeye (Sheikh). 

"Yote haya Sheikh umeyataka wewe, tulikuasa usiingie katika mambo hayo ya UWAWARU leo hii Waislamu wa Rufiji tunaitwa makafiri", alisema kwa huzuni muumini huyo. 

Kusikia maneno hayo, Sheikh naye aliangua kilio ghafla hali iliyowashangaza wengi waliokuwepo Msikitini hapo. 

Imedaiwa kuwa Sheikh Rwambo ndiye aliyewashawishi Waislamu wa Rufiji kujiunga na UWAWARU kwa kutoa fatwa zinazohalalisha ushirikiano baina ya Waislamu na Wakristo. 

Hata hivyo, pamoja na fatwa hizo za Sheikh mfululizo wa vikao vya Waislamu ulikuwa ukiendelea wilayani humo kufuatia kuundwa kwa UWAWARU ambapo kikao kingine baada ya kile cha kwanza kilifanyika Jumatano wiki hii. 

Kikao hicho kiliwahusisha Maimamu wa Misikiti yote ya Ikwiriri na waumini wengine ambapo baada ya mjadala mrefu iliafikiwa kuwa umoja huo unakiuka mafundisho ya Uislamu. 

Baadhi ya waumini waliojiunga na UWAWARU walidai kudanganywa na Wakristo kuwa iwapo wangeafiki umoja huo wangejengewa hospitali. 

"Wakatuzunguka tukajisahau, kuanzia sasa tunauvunja umoja huo", alisema Shahara aliyekuwa msemaji mkuu wa viongozi wa UWAWARU upande wa Waislamu. 

Mwishoni mwa kikao hicho iliazimiwa Waislamu wajitoe UWAWARU na kuwatenga wale wote watakaojinasibisha na umoja huo. 

UWAWARU iliasisiwa na Wamisheni waliofika wilayani hapo kwa kushirikiana na Mheshimiwa Mbonde miezi miwili iliyopita. 

Malengo ya umoja huo kwa mujibu wa Mheshimiwa Bakari Mbonde ni kujenga mahusiano mema miongoni mwa wananchi wilayani Rufiji. 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
Tahariri
Umaskini unachafua mazingira!

Mauaji ya Mwembechai: Spika wa Bunge aombwa atoe gharama za kuunda Tume

UWAWARU yafa Rufiji

UN yaidhinisha udhalimu wa Marekani

Qur’an yachomwa moto Shinyanga

Marekani yadhihirisha Ubeberu wake

MARADHI YA KISAIKOLOJIA: SEXUAL SADISM
Na. Abu Halima Sachangwa

Kitengo cha Zaka chazinduliwa Dar

Tume ya Jiji kubomoa Msikiti wa vipofu

Akheri ya zamani
Na Alhaj Yusuf Kalala, Washington DC. USA

UWAWARU yaleta nusura Ikwiriri

Tamko la Masjid NNUUR juu ya kuanzishwa kwa UWAWARU

Kuanzishwa kwa UWAWARU

Wasomi Waislamu wawajibike
Na Mwandishi Wetu

Albucasis  936 - 1013 (CE)

Ijue Uhuru madrasa - Morogoro

Madrasa Akhlaqil Islamiya yapiga hatua

MADRASATUL Husseiniyi Shadhily
Na Jamillah Nassoro
 
Hatimaye kesi ya kushambulia kituo nayo yafutwa

Changieni vyombo vya mihadhara - Sheikh Said

Misikiti yakosa maji ya kutawadhia

Bakwata Tanga haifuati katiba yake

Sheikh Mbukuzi ataka Waislamu watafute radhi za Allah

Je, hivi tuendelee kushika amri za Mungu tena? - 3
Na Mwinjilisti Bunga E. Dettu

Njia ya uzimani ni nyembamba,  waionao ni wachache - 3
Na Yasin Valerian Massawe

Sheikh Omar Bashir afikishwa mahakamani

Mufti pekee kuidhinisha watu kufunga

Nguruwe wanaofugwa maeneo wanayoishi watu kusababisha magonjwa ya kuambikiza

200 wamesilimu

Sayansi na Teknolojia 
[Kuiweka Modem kwenye Kompyuta] 
 
Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Mlo wa Daku] 
 
Tangazo 
New Book: The untold story of the Muslim struggle against British Colonialism in Tanganyika. 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtz.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita