|
|
| UN
yaidhinisha udhalimu wa Marekani’
BARAZA la Usalama la Umoja wa Mataifa limeshutumiwa kwa kuidhinisha ubabe na udhalimu wa Marekani dhidi ya mataifa mengine. Watu wengi waliotoa maoni yao kufuatia mashambulizi ya Marekani dhidi ya Iraq wamesema baraza hilo limeshindwa kuwa na msimamo pale Marekani inapokiuka sheria za kimataifa. Wamemlaumu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Kofi Annan kwa kushindwa kutoa kauli ya baraza badala yake kuelezea hisia zake binafsi. Bwana Kofi Annan amenukuliwa na vyombo vya habari akielezea masikitiko yake juu ya mashambulizi ya Marekani dhidi ya Iraq bila ya kueleza msimamo wa Baraza lake. "Hii ni siku ya huzuni kwa watu wa Iraq, ghuba na ulimwengu kwa ujumla, mimi nimejitahidi kwa kiasi kikubwa kuumaliza mgogoro huu kwa njia za amani", Katibu huyo alinukuliwa na kituo kimoja cha televisheni. Kauli hiyo ya Bwana Annan imetafsiriwa kuwa Umoja wa Mataifa (UN) haukuruhusu mashambulizi hayo ya Marekani dhidi ya Iraq. Kwa mujibu wa matangazo ya vituo mbalimbali vya televisheni, watu wawili waliuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa nchini Iraq kufuatia mashambulizi hayo. Aidha majengo kadhaa pamoja na miundo mbinu imeharibiwa vibaya na makombora yapatao 200 yaliyorushwa na majeshi ya Marekani nchini humo. Mashambulizi ya Marekani yamefanyika katika mkesha wa mjadala wa maamuzi ya kashfa ya ngono inayomkabili Rais Bill Clinton. Mjadala huo ulikuwa uamue Bill Clinton avuliwe madaraka na kushitakiwa au aendelee na Urais wa nchi hiyo. Takriban asilimia 52 ya Wamareka hawaridhii kuongozwa na Rais anayesemekana
kuliongopea taifa hilo katika kesi yake na Monica Lewinsky.
|
YALIYOMO
Tahariri Umaskini unachafua mazingira! Mauaji ya Mwembechai: Spika wa Bunge aombwa atoe gharama za kuunda Tume UN yaidhinisha udhalimu wa Marekani Qur’an yachomwa moto Shinyanga Marekani yadhihirisha Ubeberu wake MARADHI
YA KISAIKOLOJIA: SEXUAL SADISM
Kitengo cha Zaka chazinduliwa Dar Tume ya Jiji kubomoa Msikiti wa vipofu Akheri ya
zamani
UWAWARU yaleta nusura Ikwiriri Tamko la Masjid NNUUR juu ya kuanzishwa kwa UWAWARU Wasomi
Waislamu wawajibike
Madrasa Akhlaqil Islamiya yapiga hatua MADRASATUL
Husseiniyi Shadhily
Changieni vyombo vya mihadhara - Sheikh Said Misikiti yakosa maji ya kutawadhia Bakwata Tanga haifuati katiba yake Sheikh Mbukuzi ataka Waislamu watafute radhi za Allah Je,
hivi tuendelee kushika amri za Mungu tena? - 3
Njia
ya uzimani ni nyembamba, waionao ni wachache - 3
Sheikh Omar Bashir afikishwa mahakamani Mufti pekee kuidhinisha watu kufunga Nguruwe wanaofugwa maeneo wanayoishi watu kusababisha magonjwa ya kuambikiza Sayansi
na Teknolojia
Chakula
na lishe
|