|
|
| Ijue
Madrasat Riyaadhwa ya mjini Dodoma
MADRASATI Riyaadhwa ni madrasa ya mchanganyiko ambayo ipo njia panda ya Chamwino na Area C; muasisi wa madrasa hii pamoja na Msikiti wake ni mhisani Bwana Khalipha Abdallah (Hongera). Madrasati Riyaadhwa ilianzishwa Novemba 20, 1994 ikiwa na wanafunzi 6 wakiwa ni watoto wa muasisi Bwana Khalifa Abdallah (Hongera) hadi sasa madara hii ina wanafunzi 205; wavulana 155 na wasichana 50. Madrasa ina mwalimu mmoja ambaye ni Alhaj Juma Athumani akisaidiana na wanafunzi waliofikia kiwango cha juu cha elimu. Aidha, yupo Ustadh Sharif Ahmad ambaye huja kila mwezi kutoka Dar es Salaam kwa ajili ya ufundishaji wa fani za juu. Masomo yafundishwayo katika madrasa hii ni Qur’an na tafsiri yake; swarfa, Hadith, Fiqh, Tawhiid, Tasaufi, Balagha, Tarekhe na Mantiqi. Malengo ya madrasa hii kwa sasa na ya baadaye ni kutoa mafunzo ya Kiislamu, uendeshaji wa Ibada, kujenga na kuanzisha bweni, kuanzisha shule ya seminari, maktaba, zahanati na kitengo cha ufundi chereheni (ushonaji) na useremala. Pia uanzishwaji wa matawi mawili ambayo ni Mar-wa likiwa Dodoma mjini na Sakami (Riyaadhwa B) likiendeshwa na walimu watatu. |
YALIYOMO
Tahariri Hakuna Idd kwa wanafunzi Waislamu mwaka huu Baada ya wanafunzi Wakristo kusherehekea Krismasi: Wanafunzi Waislamu kuikosa Id el Fitr Hoi hoi zatawala ziara ya Mwinyi Mwanza Waislamu Tunduma waswali ndani ya kilabu cha ulanzi MARADHI YA KISAIKOLOJIA: FROTTEURISM Barabara za Tabora zimepitwa na wakati Jicho la
Uzalendo: Nihiari yetu kuendelea kujidanganya!
Kuanza na kwisha mwezi wa Ramadhani Taarifa ya Kamati juu ya yaliyotokea Mwembechai Maazimio ya kongamano la wanawake wa Kiislamu Waislamu kijijini Kidunda Moro wahitaji mwalimu Waislamu Mtwara wadai jengo la Wakfu kwa CCM Wakati Makanisa yakimeremeta: Msikiti wageuka gofu Sanya Juu Sheikh Khalifa Suleiman afariki dunia Sheikh wa wilaya ya Lushoto afariki Ijue Madrasat Riyaadhwa ya mjini Dodoma Mwinyi apongeza juhudi za kulea yatima Mwanza Tuhuma za kupindua uongozi wa Bakwata: Sheikh Hamim Boza akanusha kuhusika Kuongezeka kwa ajali za barabarani Njia ya
uzimani ni nyembamba, waionao ni wachache - 4
Saggaf awataka watoto wahifadhi Qur'an Waislamu watakiwa kujitolea kupigania dini yao Kesi nyingine Mwembechai yaahirishwa Sayansi
na Teknolojia
Chakula
na lishe
|