|
|
| Barabara
za Tabora zimepitwa na wakati
UKARABATI wa barabara mjini Tabora unaofanywa na kampuni moja kutoka China umelalamikiwa kuwa hauzingatii wakati na taratibu za mipango miji. Akizungumza na gazeti hili wiki hii, mwenyeji mmoja wa mjini Tabora aliulaumu ukarabati huo kwa kusema kuwa umepitwa na wakati. "Nauliza swali, hivi vipande vya barabara vinavyotengenezwa Tabora tumeiga nchi gani yenye barabara kama palio la ng’ombe", alihoji mwananchi huyo aliyejitambulisha kwa jina la Msigara Khalfani. Bwana Msigara ameshangazwa na jinsi barabara hizo zinavyokarabatiwa chini ya mwembe na migazi bila ya kuwepo kwa mpango maalum. Mzalendo huyo ametoa ushauri kuwa hakuna haja ya kuleta watalaamu kutoka nje ya nchi kwa gharama kubwa ambao utendaji wao hautofautiani na wataalamu wa hapa nchini. Aidha, amewaomba wahusika wa mipango miji, mjini Tabora wauweke mji huo katika mandhari ya kupendeza kama ilivyo katika miji mingi hapa nchini. Tabora ni moja ya miji mikongwe hapa nchini ambapo historia yake inajitokeza zaidi katika harakati za kudai uhuru wa nchi hii miaka ya 1940 hadi 1961. Mji huo hadi hivi una kiwanda kimoja tu ambacho huenda kikafa wakati wowote kutokana na uzalishaji wake duni. Hali ya maisha ya wakazi mjini ni ya chini sana, vijana wengi wameukimbia mji huo na kwenda mikoa ya kanda ya ziwa na pwani. Barabara ya Mwanza ambayo ilikuwa maarufu enzi hizo hivi sasa imechakaa mno kiasi cha kupoteza umaarufu huo. Nyumba za matope ndizo zilizo nyingi katikati ya mji huo na pembezoni mwake. Wito umetolewa kwa wenyeji wa mkoa huo kutafakari sababu zilizopelekea mkoa huo kusonga nyuma miaka 37 sasa na hatua za kuchukua ili kurekebisha hali hiyo kwa kuzingatia uchaguzi ujao.
|
YALIYOMO
Tahariri Hakuna Idd kwa wanafunzi Waislamu mwaka huu Baada ya wanafunzi Wakristo kusherehekea Krismasi: Wanafunzi Waislamu kuikosa Id el Fitr Hoi hoi zatawala ziara ya Mwinyi Mwanza Waislamu Tunduma waswali ndani ya kilabu cha ulanzi MARADHI YA KISAIKOLOJIA: FROTTEURISM Barabara za Tabora zimepitwa na wakati Jicho la
Uzalendo: Nihiari yetu kuendelea kujidanganya!
Kuanza na kwisha mwezi wa Ramadhani Taarifa ya Kamati juu ya yaliyotokea Mwembechai Maazimio ya kongamano la wanawake wa Kiislamu Waislamu kijijini Kidunda Moro wahitaji mwalimu Waislamu Mtwara wadai jengo la Wakfu kwa CCM Wakati Makanisa yakimeremeta: Msikiti wageuka gofu Sanya Juu Sheikh Khalifa Suleiman afariki dunia Sheikh wa wilaya ya Lushoto afariki Ijue Madrasat Riyaadhwa ya mjini Dodoma Mwinyi apongeza juhudi za kulea yatima Mwanza Tuhuma za kupindua uongozi wa Bakwata: Sheikh Hamim Boza akanusha kuhusika Kuongezeka kwa ajali za barabarani Njia ya
uzimani ni nyembamba, waionao ni wachache - 4
Saggaf awataka watoto wahifadhi Qur'an Waislamu watakiwa kujitolea kupigania dini yao Kesi nyingine Mwembechai yaahirishwa Sayansi
na Teknolojia
Chakula
na lishe
|