|
|
Njaa
yaikumba Kilwa
Hali ya chakula mjini Kilwa ni mbaya ambapo baadhi ya watu huponea maembe na mizizi ya miti. Mwandishi wa habari hizi alishuhudia baadhi ya Waislamu waliofunga wakifuturu maembe ya kuchemsha nyakati za magharibi. Njaa imeathiri maisha ya watu na wanyama na katika baadhi ya maeneo nyani wamekuwa wakivamia nyumba na kuipua vyungu jikoni. Maeneo ambayo yameathirika zaidi ni pamoja na Migelegele, Luhatwe, Kikale, Mitole, Njinjo na Nshotike ambako mwandishi alishuhudia makopa ya maembe yaliyoanikwa juani. Baa la njaa huenda likasababisha maafa zaidi baada ya msimu wa maembe kwisha, iwapo jitihada za makusudi hazitachukuliwa kuwanusuru wananchi wa wilaya hiyo. Kwa miaka miwili mfululizo wilaya ya Kilwa na vitongoji vyake imekuwa ikikumbwa na majanga mbalimbali ikiwa ni pamoja na njaa na mafuriko. Mwaka 1997 Kilwa ilikumbwa na njaa iliyosababishwa na mafuriko yaliyoharibu mazao na nyumba kadhaa pamoja na kupoteza maisha ya watu wengi. Wananchi wilayani hapa wamekuwa wakiilalamikia serikali kwa kutochukua hatua za dharura kuwasaidia kukabiliana na majanga hayo. Wananchi hao wamesema viongozi wa serikali huonekana sehemu hizo nyakati za uchaguzi. Wakati huo huo, huku wananchi katika baadhi ya mikoa wakiendelea na maadhimisho ya kuukaribisha mwaka mpya 1999 na kuuaga mwaka 1998, mikoa ya Dodoma, Ruvuma, Lindi na Mtwara iko katika njaa kubwa. Taarifa kutoka mikoa hiyo zinafahamisha kuwa kuna uhaba mkubwa wa chakula
ambao huenda ukasababisha maafa kwa wakazi walio wengi.
|
YALIYOMO
Tahariri Kingunge, kweli upo uonevu na dhulma Wananchi wahoji kuhusu polisi aliyeua Arusha Dondoo za Saikolojia
Kona ya Wacha Mungu
Jicho la Uzalendo: Bhabhoo! Muungwana
huyoo!
Maulana Sayyid Jamal-Din Afghan 1214 - 1254 (1838-1897) Mafunzo kuhusu funga ya Ramadhani
Marekani ni mtetezi au adui wa haki?:
Umoja wa Mataifa upo upande gani?
Dawa ya ukimwi ni mwenendo mwema
Mwalimu Maif: Mwanamke aliyetumia maisha yake kufundisha Qur'an Wazazi waaswa kutoshabikia maovu Je, hivi tuendelee kushika amri za
Mungu tena? (jibu)
Mapinduzi, Muungano kwa manufaa ya nani? Fufueni EAMWS - Sheikh Amana
Msiitupie lawama serikali - Dk. Omar Baada ya kuvunjiwa nyumba,
kuchomewa vyakula na Serikali: Nzasa sasa wafuturu Maembe
Acheni mifumo mibovu, fuateni Qur'an - Sheikh Kilemile Sayansi na Teknolojia
Chakula na lishe
|