|
|
Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Ustaadh Yunus Abdallah katika Msikiti wa Merela Morogoro vijijini alipokuwa akiwahutubia Waislamu wa tarafa ya Merela katika sala ya Ijumaa kufuatia Waislamu kadhaa wa tarafa hiyo kuritadiwa wakisaidiwa na "Sheikh" wao ambaye aliomba msamaha baadaye kwa madai kuwa "alighafirika". Hata hivyo, uchunguzi wa gazeti hili uligundua kwa kadhia hiyo ilitokana na uchache wa elimu sahihi ya Uislamu tarafani hapo. Akiuweka wazi ukweli wa mambo, Ustadh Yunus ambaye ni mmoja wa viongozi waandamizi wa vijana wa Msikiti wa Kiwanja cha Ndege mjini hapa, alisema kwamba wasomi wa Kiislamu mjini Morogoro wana dhima kubwa ya kujibu mbele ya Allah (s.w.) kwani hawatumii vilivyo elimu yao kwa manufaa ya Uislamu na Waislamu kiujumla, badala yake wanaitumia kwa maslahi yao binafsi jambo ambalo ni hujuma chafu dhidi ya Uislamu. "Tumeachana na Qur’an na Sunnah za Mtume (s.a.w.) na kufungua kitabu kipya cha malumbano ya kiitikadi, kitendo ambacho maadui wa Uislamu wanakitumia vizuri kutudidimiza", alisema kijana huyo. Aidha, Ustadh Yunus aliwaonya wasomi hao kuwa kuwagawa Waislamu kwa vigezo vya ukabila hasa Ukigoma kwa upande mmoja na Uruguru au "Tuimanye" kwa upande mwingine. "Waislamu ni kitu kimoja, si rangi, kabila, jinsia, hali zao kiuchumi au kimaumbile (walemavu na wazima) ndizo zinazotambulisha umoja wao, bali Allah (s.w.) wa pekee", alisema. Akiwaelezea matajiri wa Kiislamu wa mjini hapa, kiongozi huyo wa vijana aliwaeleza wazi kuwa utajiri wao hauna mashaka yoyote kwa Uislamu, kinyume chake unawanufaisha wasio kuwa Waislamu kwa kuwajengea mashule na vyuo vikuu. Naye Ustadh Mohammed Kisanda akizungumza katika ziara hiyo aliwataka Waislamu wa vijijini kuzama katika elimu sahihi ya Uislamu na akawaonya wasithubutu kuigawa elimu katika matapo mawili (elimu dunia na akhera). "Tukipuuza elimu au kuigawa, majengo ya madrasa zetu hata Misikiti si
muda mrefu itageuzwa maghala ya kuhifadhia pamba na mpunga", alionya Ustadh
Kisanda
Abiria walaani kumwagiwa pombe Kondoa ABIRIA waliokuwa wakisafiri katika basi la Champion Bus Service kutoka Kondoa kwenda vijiji vya Mondo, Simba Songolo hadi Soya walipatwa na hasira pale waliponajisiwa nguo zao na pombe kutokana na kupasuka kwa chupa. Tukio hilo lilitokea hivi karibuni katika kituo cha mabasi mjini Kondoa, wakati kondakta wa basi hilo Bwana Sabiiku alipomwamuru utingo wake aliyejulikana kwa jina la Nuuri kupakia kreti mbili za bia aina ya Safari Lager. Katika harakati hizo, kreti moja iliponyoka na chupa kuvunjika juu ya keria ya basi hilo na pombe kuanza kuwaloanisha abiria, kitendo hicho kilaaniwa vikali na Watu waliokuwa ndani ya basi hilo. Watu hao walichukuzwa zaidi na kitendo hicho hasa kwa kile mmiliki wa basi hilo ni Muislamu, hata heshima ya mwezi mtukufu hakuna, alidai Bwana mmoja, Aidha, Sheikh Suleiman Mhunzi aliitumia nafasi hiyo kwa kuwaeleza abiria kuwa si kwa mnywaji wa pombe aliyelaaniwa hata yule mwenye kuibeba na kutumia kipato chake nao wamelaaniwa vile vile. Mwandishi wa habari hizi aliyekuwa ndani ya gari hilo alimsikia kondakta
Bwana Sabiiku akimuamrisha utingo wake achukue maji na kufuta sehemu hiyo
ya mlangoni hatua ambayo haikusaidia kwani abiria waliokaa mlangoni walikuwa
wamelowanishwa.
CHAMA kipya cha waandishi wa habari wa kujitegemea Morogoro (MFJA) kimemteua Sheikh Mkuu wa Mkoa Sheikh Omar Bafadhil kuwa mmoja wa wadhamini wake mwishoni mwa wiki katika uchaguzi mkuu wa chama hicho uliofanyika katika ofisi za muda za chama hicho zilizopo barabara ya Stesheni mjini hapa. Aidha, uliwateua wadhamini wengine wanne ambao ni pamoja na Bwana Idan Hassan Libenanga, meneja wa TTCL Morogoro, Bwana Bendera Mwenyekiti wa bodi ya maji mkoa, Bw. Petro Kingu na Mwenyekiti wa chama cha soka mkoa Bw. Aman Komanya. Pia mkutano umemchagua Bw. Boniventura Mtalimbo kama Mwenyekiti wake akisaidiwa na Bw. Thadei Hafigwa. Wengine ni Bwana Seraph Kuandika aliyechaguliwa kuwa Katibu Mkuu akisaidiwa na Bwana Rajab Rajab. Bi. Gladness Mushi alichaguliwa kuwa Mweka hazina akisaidiwa na Bwana Gaudence Masati, wakati Bwana Mussa Ally na Bi. Jamila Malinza walichaguliwa kuwa wajumbe wa kamati hiyo ya utendaji itakayoongoza chama hicho kwa kipindi cha miaka miwili ijayo. MFJA imeundwa kwa lengo la kusimamia maslahi, kutetea haki, kuwaunganisha na kuwaendeleza kitaaluma waandishi wa habari wa kujitegemea mkoani Morogoro. Wakati huo huo, wito umetolewa kwa vijana wa Kiislamu wenye elimu ya kutosha kujiunga na taaluma ya uandishi wa habari ili kuutetea na kuuendeleza Uislamu na Waislamu kiujumla. Wito huo umetolewa hivi karibuni na Waislamu wa mjini hapa walipoongea na gazeti hili kwa nyakati tofauti kufuatia pengo lililoonekana hasa mjini Morogoro ambapo Uislamu na Waislamu hususan vijijini wanaelekea kaburini kimaendeleo bila ya ulimwengu wa Kiislamu kujua kutokana na ukosefu wa waandishi wa habari wa Kiislamu mjini hapa. Hadi hivi sasa waandishi wa Kiislamu mjini Morogoro hawazidi wawili, jambo ambao ni msiba mkubwa kwa ulimwengu wa habari za Kiislamu. |
YALIYOMO
Tahariri Onyesheni ushujaa wa Badri Daniel kuwatimua waumini Msikitini Waislamu Moshi: Wadai kulishwa nguruwe, vibudu Dondoo za Kisakolojia
Maulana Sayyid Jamal-Din Afghan 1214 - 1254 (1838-1897) - 2 MASHAMBULIZI YA MAREKANI NCHINI IRAQ Njia bora zitakazotusaidia kuwalea
watoto
Ijue Madrasatul-Qaadiriya Sokoni
I Arusha.
Tutafute kwanza ufalme wa Allah (s.w.)
Chuo cha Kilimo Ukiriguru kupata
Msikiti mpya
Huduma za maji Kondoa haziridhishi
Mnyororo wa imani
Je, Yesu alibatizwa?
Kufuatia Waislamu kuritadishwa Merela Morogoro: Masheikh wa mjini watupiwa lawama Abiria walaani kumwagiwa pombe Kondoa Sheikh Bafadhil ateuliwa
kudhamini waandishi wa habari Morogoro
Sayansi na Teknolojia
Chakula na lishe
|