|
|
| Kona
ya WachaMungu
Udugu wa kweli huja pale ... NAJARIBU kufikiria hatua ambazo ningechukua kuuimarisha udugu wetu wa imani kama ambavyo Allah(s.w) anavyotuhimiza katika Qur’an. Udugu ninaouona hapa si ule ambao wengi wangeudhani. Ni udugu unaokuja baada ya kutekelezwa masharti kadhaa pia kuzingatia miiko yake. Kwa mujibu wa mafunzo ya Mtume(s.a.w) Waumini tunajifunza baadhi ya yanayoweza kujenga udugu wa kweli wa kiimani na pia kuyajua yanayotishia udugu huo. Mtume (s.a.w.) amesema peaneni salamu mtapendana. Pia amehimiza kutembeleana, kualikana, kuandaliana vyakula. Hili Waislamu wengi wamekuwa wakitekeleza Alhamdulillah! Hata hivyo, Salaam na kutembeleana ni makapu yaliyokusanya mambo mengi ndani yao. Uhakika ni kwamba haiyumkini ibakie salaam iliyosisitizwa na Mtume; wakati ameficha chuki, choyo, utesi, masengenyo, majivuno, kashfa, dharau na kero nyingine. Na hakuyumkini kutembeleana kulikohimizwa na Mtume (s.a.w.) ilhali kumeandamana na husda, wivu, ria, kukogana na mengine yaliyojificha katika mitihani ya kupata na kukosa. Hayupo katika udugu wa Kiislamu yule ambaye atatoa "salaam alaykum" kwa "nduguye" Muislamu kwa dakika hii kisha dakika nyingine akae na kumzungumza vibaya nduguye huyo, iwe chemba na wale wa karibu zaidi nae au na mke au mumewe nyumbani kwani huu unaangukia kwenye usengenyi na utesi ambayo ni kansa inayoozesha viungo vya mafungamano ya Uislamu. Wengi tunaopanga safu za jamaa Misikitini tulio mstari wa mbele katika makundi na "harakati", tunaugua ugonjwa huu! Hayupo katika udugu wa Kiislamu yule ambaye "asalam alaykum" imetawala kinywa chake wakati nduguze katika imani wanaendelea kutaabika kwa hali ngumu kimaisha ilhali anao wasaa ... Si katika salamu iliyohimizwa na Mtume (s.a.w.) ile inayotoka katika kinywa cha asiyeguswa na matatizo ya wengine. Tushindane kuyafikia mambo ya kheri yanayoboresha udugu miongoni mwetu yasiyotoa mianya kwa mashetani wanaoweza kujipenyeza kwa sura tofauti kihali na kimali. Na tukumbuke kuwa udugu wa kweli miongoni mwa waumini ni Faradhi: "Hakika waumini wote ni ndugu". (49:10)
Jicho la Uzalendo Ukombozi umeegemea kwenye kafara! MALALAMIKO na vilio vya wananchi Waislamu wa nchi hii juu ya kero mbalimbali zinazowakabili, vimekuwa vikiambulia patupu mara kadhaa. Hii si kwamba wahusika hawaoni au kusikia, la hasha! Wanasikia na kukiri ukweli wa hayo, lakini jambo moja laelekea kuwa ndio ni kwamba kwa kuwa katiba si zao la muafaka, hukuwepo wewe, mimi wala yule wakati "ikitengenezwa", kwa hiyo, huwezi kumfanya lolote anayekutenda visivyo katika walio juu kinchi. Labda utumie mbavu zako. Wakati Katiba ikiwa katika mazingira ya "mizengwe" kiasi hicho, pia kuna wale waliokosa uzalendo unaojali ustawi wa wote! Hawa wamekosa shukrani na uungwana baada ya kutua kivulini. Hawataona haya kufanya yao pasi na kuzingatia uwepo wa wengine. Kinadharia hula kiapo kuwa watendaji chini ya Katiba, kiutendaji mara kadhaa hutenda kwa mujibu wa maelekezo yasiyo rasmi ya watakatifu wao. Kibaya zaidi, kwa hawa, huwa watiifu kwa asilimia mia moja! Kukaa na kuamua kumsaka Ponda au kuwashitaki walioko mahakamani hivi sasa kuhusu Mwembechai huku ukimwacha , mchochezi Paroko wa Mburahati ni katika hayo tunayodhani ya kutekeleza maagizo yasiyo rasmi. Kuahirisha mitihani au matokeo ili kusherehekea vyema Krismasi huku ukiwasahau wanaofunga na kutarajia kusherehekea Idi ni katika hayo ya Katiba kutokuwa na wajibu wowote katika jamii yetu. Na haya yanakuja kwa sababu walioko juu hawategemei wala hawatokani na nguvu ya wananchi (kura). Uwachague watakuwepo, usiwachague watakuwepo. Mataifa ambayo wananchi wake huwa na kauli, tunayaona yaking’ara kisiasa. Viongozi huheshimu maamuzi ya Wananchi, husikiliza malalamiko na vilio vyao. Hujibu tuhuma dhidi yao na hutatua shida zao. Upendeleo, chuki, mizengwe ya udini, dharau na ubabe havina nafasi. Huku kwetu haya ni ndoto kwa baadhi ya wananchi kwa sababu viongozi wana uhakika wa kushinda hata kama nchi nzima hawatapiga kura! Katika hali na mazingira haya ya kutotendewa haki kwa baadhi ya wananchi, ufumbuzi utapatikana pale tu hawa wanyonge watakapojiona wanastahiki kupata kila kilicho chao kwa gharama yoyote! Mimi sikubaliani na wale wanaohimiza
"utangamano" katika mazingira haya. Huo ni unafiki, huko ni kulinda maslahi
ya waporaji wachache wa haki za wengi. Naona ukombozi umeegemea zaidi kafara
ya damu.
|
YALIYOMO
Tahariri Onyesheni ushujaa wa Badri Daniel kuwatimua waumini Msikitini Waislamu Moshi: Wadai kulishwa nguruwe, vibudu Dondoo za Kisakolojia
Maulana Sayyid Jamal-Din Afghan 1214 - 1254 (1838-1897) - 2 MASHAMBULIZI YA MAREKANI NCHINI IRAQ Njia bora zitakazotusaidia kuwalea
watoto
Ijue Madrasatul-Qaadiriya Sokoni
I Arusha.
Tutafute kwanza ufalme wa Allah (s.w.)
Chuo cha Kilimo Ukiriguru kupata
Msikiti mpya
Huduma za maji Kondoa haziridhishi
Mnyororo wa imani
Je, Yesu alibatizwa?
Kufuatia Waislamu kuritadishwa Merela Morogoro: Masheikh wa mjini watupiwa lawama Abiria walaani kumwagiwa pombe Kondoa Sheikh Bafadhil ateuliwa
kudhamini waandishi wa habari Morogoro
Sayansi na Teknolojia
Chakula na lishe
|