|
|
|
Susieni mitihani Ndugu Mhariri VYOMBO vya habari vimetangaza kuwa Wizara ya Elimu imechelewesha kutoa matokeo ya Darasa la Saba ili watoto wa Kikristo waweze kusherehekea Krismasi. Yaani Wizara ya Elimu haikutaka kuwaudhi Wakristo katika sikukuu ya Krismasi na Boxing Day. Hapo hapo Wizara hiyo hiyo imetangaza tarehe ya kurudiwa mitihani ya Kidato cha Nne ambayo itaanza tarehe 13 Januari 1999 wakati watoto wa Kiislamu wote watakuwa wamefunga swaumu ya Ramadhani na watasherehekea sikukuu ya Idd wakiwa katika mitihani au watakuwa na "Examination Fever" (kitete cha mitihani) wakati wakisherehekea Idd. Serikali ya Tanzania kwa mara nyingine tena imeonyesha upendeleo wa wazi kabisa kwa Wakristo kusherehekea Krismasi na Boxing Day bila ya huzuni na hapo hapo kuwaacha Waislamu wataabike na Mitihani ndani ya Ramadhani na sikukuu ya Idd. Natoa mwito kwa vijana wa Kiislamu Tanzania Bara wasusie mitihani hiyo hadi baada ya Idd. Vile vile TAMSA, DAMUSA na jumuiya nyingine za wanafunzi wa Kiislamu mikoani itoe msimamo juu ya kadhia hii. Ikiwa vijana wote wa Kiislamu watasusia mitihani hiyo tunahakika serikali italiona jambo hili kuwa ni zito na linafaa kutizamwa upya. Hapo hapo TAMSA na DAMUSA isipotoa kauli na msimamo basi nayo ivunjwe kwani itakuwa ipo hapo ilipo kwa manufaa ya wasio Waislamu. Abu Khalid Wa Hussein,
Waislamu Rufiji wamenishangaza Ndugu Mhariri NINAOMBA fursa hii kwa mara yangu ya kwanza katika gazeti letu tukufu ili niweze kuufikisha ujumbe wangu kwa ndugu zetu Waislamu wa Rufiji. Katika gazeti hili, toleo nambari 176 ukurasa wa 15 (kumi na tano) kulikuwa na kichwa cha habari "Waislamu, Wakristo Rufiji watakiwa kuunda umoja". Kilichonishangaza zaidi ni kwamba katika toleo nambari 179 ukurasa wa kwanza kuna picha ya pamoja ya viongozi wa umoja huo (Uwawaru); hii inaonyesha kwamba tayari ndugu zetu hawa wameshakubali kujiunga na Wakristo hao. Kwa maana hiyo wameshaamini na imani yao ya kuwa Mungu ana nafsi tatu na kuwa Yesu (Isa bin Mariam) ni mungu, mwana wa Mungu na amesulubiwa msalabani. Wakati katika imani ya Kiislamu sio kweli kabisa. Inaelekea ndugu zetu hawa wamesahau maneno ya Mwenyezi Mungu (s.w.) katika kitabu chetu kitukufu (Qur’an) naomba niwakumbushe kwa kurejea aya zifuatazo: Mwenyezi Mungu (s.w) anasema: "Enyi mlioamini! Msiwafanye wasiri wenu watu wasiokuwa katika nyinyi hao hawataacha kukufanyieni ubaya. Wanayapenda yale yanayokudhuruni. Bughudha (yao juu yenu) inadhihirika katika midomo yao. Na yanayofichwa na vifua vyao ni makubwa zaidi. Tumekubainishieni dalili (zote) ikiwa ni nyinyi ni watu wa kufahamu". (3:118). Oh, nyinyi mnawapenda (maadui zenu hao) hali wao hawakupendeni. Nanyi mnaamini vitabu vyote (chenu na vyao). Na wanapokutana nanyi husema "Tumeamini". Lakini wanapokuwa peke yao wanakuumieni vyanda kwa chungu (wa kukuchukieni) sema kufeni kwa uchungu wenu (huo), hakika Mwenyezi Mungu anayajua (hata) yaliyomo vifuani". ( 3:419). "Ikikupateni kheri huwasikitisha ila ikikupateni shari wanaifurahia. Na kama nyinyi mkisubiri na mka mcha Mungu hila zao hazitakudhuruni kitu. Hakika Mwenyezi Mungu anayajua vizuri yote wanayoyatenda". (3:120) "Enyi mlioamini! Msiwafanye Mayahudi na Wakristo kuwa marafiki. Na miongoni mwenu atakayefanay urafiki huo nao; bali huyo atakuwa pamoja nao. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongozi (njia ya kheri) watu madhalimu". (5:5) "Enyi mlioamini! Msiwafanye marafiki wale alioifanyia mzaha na mchezo dini yenu miongoni mwa wale waliopewa kitabu kabla yenu na miongoni mwa makafiri (wengine). Na mcheni Mwenyezi Mungu kama nyinyi ni wenye kuamini". (5:57) Kutokana na aya hizo hapo juu, mimi naungana na Sheikh Jongo kwa kuichachamalia Uwawaru na kuwaomba viongozi wa kidini kuweza kuchukua hatua za kuwasaidia ndugu zetu wa Rufiji Insha-allah Mwenyezi Mungu awawezeshe kurejea. Namalizia kwa kuwaomba Waislamu wa Rufiji warejee aya zilizotajwa hapo juu, wazitafakari na wazifanyie kazi Insha-Allah. Sharifa Yusuf,
Kwanini Waislamu tumepoteza maadili yetu Ndugu Mhariri NAOMBA nafasi katika gazeti lako hili mahiri nitoe machache kuhusiana na kichwa cha habari hapo juu Insha-Allah. Napenda kuwakumbusha Waislamu kwa ufupi kuhusiana na kupoteza maadili yao (kupotea mwelekeo tulioachiwa na Mtume (s.a.w.) kama alivyoamrishwa na Allah (s.w.) atufikishie na yeye amefufikishia). Kwanini Waislamu tumeupoteza ule Uislamu tuliofundishwa na Mtume (s.a.w.) na vipi tutaurejesha kama ulivyo kuwa. Waislamu tumepoteza maadili (mwelekeo) wa dini hii, Waislamu hatuna umoja, tumejigawa makundi kwa makundi na kujengeana uadui sisi kwa sisi, hali yakuwa tumeisahau kauli ya Allah (s.w.) isemayo: Na shikamaneni katika kamba ya Allah (s.w.) wala msiachane. (Qur. 3:103). Kujigawa kwetu makundi hatutaiepuka adhabu (moto) kwa Allah (s.w.) kama alivyosema Allah (s.w.) kuwa: "Tumeiteremsha adhabu kwa wale waliojigawa makundi". (Qur. 15:90). Kufuatana na aya hii ni vipi tumejigawa makundi? Tujiulize katika maisha ya Mtume (s.a.w.) yalikuwepo makundi kama haya tuliyojiundia sisi. Hii inaonyesha tumepoteza Uislamu na maadili yake, sheria na Tawhiid, kwa kuwafuata makafiri kama walivyojigawa makundi mengi (vyama). Na sisi tunajiita Waislamu tumekuwa miongoni mwa makafiri. Kwa nini tuwe miongoni mwa makafiri? Amesema Mtume (s.a.w.): "Atakayeishi muda mrefu (maswahaba) ataona mambo mengi ya uzushi na jiuepusheni nayo". Kauli hii ya Mtume (s.a.w.) imetimia maana ummah huu wa Kiislamu umetopea katika uovu na uzushi kama tunavyoshuhudia Waislamu kujigawa katika makundi na kujengeana uhasama na kupoteza umoja wao wa Kiislamu. Huu ndio Uislamu aliotufundisha Mtume (s.a.w.). Huu si Uislamu aliotufundisha Allah (s.w.) kupitia kwa mjumbe wake. Nani ataunusuru Uislamu (dini hii ya Mwenyezi Mungu). Mko wapi wanavyuoni wa Kiislamu, viongozi wa Kiislamu, Masheikh, Maimam na Waislamu kwa ujumla katika kuinusuru dini ya Allah (s.w.). Hii ni dhamana kubwa mbele yetu tuliyopewa na Allah (s.w.) kwa kuinusuru dini yake kama alivyosema: "Ni nani atakayeinusuru dini hii". (Qur. 61:14). Dhamana tuliyoyopewa ni Uislamu kama
anavyotuambia Mwenyezi Mungu: "Tumekuridhieni Uislamu kuwa dini yenu".
(Qur. 5:3). Ni vipi tumeuacha Uislamu ambao ndio Allah (s.w.) ameturidhia,
tutaunusuruje Uislamu kama hatujapoteza maadili yetu.
Kususia mazishi Masheikh tupeni fat’wa Ndugu Mhariri NAPENDA kutoa maoni yangu kuhusiana na habari iliyoandikwa katika gazeti la AN-NUUR Na. 181 Ramadhani 1419 Desemba 25-31, 1998 iliyokuwa na kichwa cha habari "Maiti ya Muislamu yasusiwa". Japo suala hili linaonekana kama ni geni kwa baadhi ya wasomaji, ukweli ni kwamba ni suala linatokea sehemu mbalimbali likiwa na mantiki ile ile ya kususia mazishi, japo laweza kuwa na sura tofauti. Kwa wenzetu wa Makole Kwafungo Tanga suala ni kuwa marehemu alikuwa "Tar kuswalat" huko kwingineko nilikokumbana nalo lilikuwa marehemu alikuwa "mlevi" au alikuwa "mchawi" ama ahudhurii mazishi ya wenzake au alikuwa na vimada n.k. La kushangaza ni kwamba viongozi hawa wamekuwa hawatupi aya au Hadith zilizobainisha ukweli wa ususiaji mazishi katika Uislamu. Hisia zangu zinanituma kuwa huenda kufanya hivyo ni sahihi ama ni chuki binafsi ama uelewa mdogo wa suala hili kidini kwa baadhi yetu. Ili kuwa na msimamo mmoja unaotokana na mwongozo wa dini ya Kiislamu, na ili kuepusha migongano itokanayo na uelewa mdogo, napenda kuwaomba wanazuoni, Masheikh na wote waliobobea, watupe msimamo wa dini kwa kuangalia aya za Qur’an na Hadith mbalimbali kuhusiana na "ususiaji mazishi". Awadh Kimito,
Uovu umekithiri Ndugu Mhariri KUNA mtindo umezuka hapa Moshi mjini wa kuwapoteza watu katika kuvutia biashara yao haramu ya kamari wanadiriki hata kusema eti Uislamu umeruhusu kamari. Napenda kuuliza ni Uislamu upi umeruhusu kucheza kamari? Na ni Uislamu upi umekataza kucheza kamari? kwani Mwenyezi Mungu ameshatukataza katika surat Al Maida aya ya 90. Ameipata wapi hiyo aya inayoruhusu kamari? Ama kweli binadamu tumepotea na kupotezwa kuliko dhahiri. Tumuombe Mwenyezi Mungu atuepushe na shaitwani, kwani yeye ni adui aliye dhahiri. Siraju Mwanga,
|
YALIYOMO
Tahariri Onyesheni ushujaa wa Badri Daniel kuwatimua waumini Msikitini Waislamu Moshi: Wadai kulishwa nguruwe, vibudu Dondoo za Kisakolojia
Maulana Sayyid Jamal-Din Afghan 1214 - 1254 (1838-1897) - 2 MASHAMBULIZI YA MAREKANI NCHINI IRAQ Njia bora zitakazotusaidia kuwalea
watoto
Ijue Madrasatul-Qaadiriya Sokoni
I Arusha.
Tutafute kwanza ufalme wa Allah (s.w.)
Chuo cha Kilimo Ukiriguru kupata
Msikiti mpya
Huduma za maji Kondoa haziridhishi
Mnyororo wa imani
Je, Yesu alibatizwa?
Kufuatia Waislamu kuritadishwa Merela Morogoro: Masheikh wa mjini watupiwa lawama Abiria walaani kumwagiwa pombe Kondoa Sheikh Bafadhil ateuliwa
kudhamini waandishi wa habari Morogoro
Sayansi na Teknolojia
Chakula na lishe
|