AN-NUUR 
Na.184 Ramadhan 1419, Januari 15 - 21, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Rais Mkapa kuwa mgeni rasmi Baraza la Idd
 
  • Apokea malalamiko ya Waislamu
  • Ukurasa mpya kufunguliwa?
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Benjamin William Mkapa huenda akawa mgeni rasmi katika Baraza la Idd litakalofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubi 
lee mapema wiki ijayo. 

Kwa mujibu wa taarifa ambazo gazeti hili imezipata, Rais pamoja na mambo mengine huenda akazungumzia malalamiko mbalimbali ambayo Waislamu wamekuwa wakiyatoa dhidi ya serikali yake. 

Utaratibu wa viongozi wa serikali kuhudhuria hafla za kidini ni wa kawaida hapa nchini ambapo katika awamu mbili za mwanzo viongozi wa kitaifa walitumia fursa hizo kujenga mahusiano ya karibu na waumini wa dini mbalimbali. 

Miaka ya mwanzo baada ya nchi kupata uhuru, aliyekuwa Rais wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere alikuwa akihudhuria hafla mbalimbali za waumini ikiwa ni pamoja na Mabaraza ya Idd ambapo kumbukumbu zinaonyesha kwamba mwaka 1970 alihudhuria Baraza la Idd el Fitr katika ukumbi wa Diamond Jubilee. 

Katika Baraza hilo Masheikh walimtakia Mwalimu Nyerere maisha marefu ili kumwezesha kuiongoza Tanzania na hatimaye kufikia lengo la Taifa la kujenga ujamaa. 

Katika awamu ya pili utaratibu huo uliendelezwa na kustawishwa zaidi ambapo Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi alihudhuria hafla hizo ikiwa ni pamoja na kufungua Misikiti na Makanisa sehemu mbalimbali nchini. 

Katika hotuba zake kwenye hafla hizo, Mzee Mwinyi alikuwa akijibu maombi, madai, malalamiko na tuhuma mbalimbali za wananchi dhidi ya utendaji wa serikali yake. 

Jumatano ya wiki iliyopita Mh. Rais Benjamin William Mkapa alikutana na Masheikh wa Dar es Salaam ambapo alipokea malalamiko na maoni ya Waislamu juu ya mambo kadhaa. 

Taarifa zimeeleza kuwa baadhi ya mambo Mh. Rais aliahidi kuyashughulikia mara moja ambapo mengine yaliahirishwa kutafutiwa muda muafaka wa mazungumzo zaidi. 

Mh. Rais alikutana na Masheikh hao Ikulu alipoandaa futari kwa ajili yao kama ilivyo ada yake kila mwaka. 

Sheikh mmoja aliyehudhuria futari hiyo ambayo baadhi ya watu wameibatiza na kuiita "ya nguvu" ameliambia ANNUUR kwamba tofauti na miaka ya nyumba futari ya mwaka huu imekuwa na tija kubwa. 

Kwanza amedai imewahusisha Waislamu toka taasisi mbalimbali, jambo ambalo limeondosha hisia kwamba wapo Waislamu wa taasisi fulani tu wanaotambuliwa na serikali. Pili amesema kwamba zaidi ya futari ilipatikana fursa ya kuongea na Mh. Rais juu ya masuala mazito yanayowagusa Waislamu ambayo Mh. Rais aliahidi kuyashughulikia. 

Hata hivyo, Sheikh huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini hakufafanua ni masuala gani yalizungumzwa na tija inayotarajiwa. 

Naye Makamu wa Rais, Dk. Omar Ali Juma amekuwa akiandaa futari kwa makundi ya Waislamu toka Jumuiya na Taasisi mbalimbali ambapo pia ilipatikana fursa ya kupeana nasaha. 

Katika moja ya nasaha zake, Mh. Dk. Omar alihimiza suala la umoja miongoni mwa Waislamu. 
 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
Tahariri 
Baada ya futari nzuri: Tuwatupie macho wenye njaa 

Rais Mkapa kuwa mgeni rasmi Baraza la Idd 

Ubungo yakumbwa na ukame 

Waumini, Masheikh Arusha wasutana kwa futari ya Mrema 

Dondoo za saikolojia 
Na. Abu Halima Sa Changwa 

Waislamu turejee kwa Allah 

MSADAT yazidi kutia moyo Tanga 

Mjue Usama bin Ladin 

MAFUNZO KUHUSU FUNGA YA RAMADHANI 

Michezo isiyoruhusiwa katika Uislamu 

Ustadh Farid: Kijana aliyejitolea kuwapa Da'awa watalii 

Hakuna Magharibi wala Mashariki: Uislamu ni ubinaadamu 
Na Abubakari S. Marwillo 

Ijue madrasati Mar-wa ya Dodoma mjini 
Na Abu Zuberi, Dodoma 

Ijue Madrasat Jadidul Fiqhyyat - Tabata Kimanga 
Na B. Mwakangwale 

Madrasat Hidayatul Muumini Mwadui 

Washindi wa mashindano ya Hadithi za Mtume (s.a.w.) wapatikana 

Madrasa Shafii Ujiji Kigoma yaonyesha umahiri wake 

Waanzisha mifuko kusaidia wagonjwa Dodoma 

Waislamu Kondoa waomba msaada kumalizia Msikiti 

Mnyororo wa imani-2 
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa 

Kutoka magazeti ya zamani: 
Wanaoshitakiwa kwa uhaini kortini leo 

Jengo la Waislamu Moshi lageuzwa Kanisa la Walokole 
Na Mwandishi Wetu, Moshi 

Masjid Nurania yaswaliwa Ijumaa 
Na Rajab Rajab, Morogoro 

Jabal Hira kutoa mafunzo ya Kompyuta Morogoro 
Rajab Rajab na Mussa Ally, Morogoro 

Sayansi na Teknolojia 
[Internet ni nini?] 

Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Thamani ya mlo wa Uyoga] 
 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtz.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita