AN-NUUR 
Na.184 Ramadhan 1419, Januari 15 - 21, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Ubungo Yakumbwa na ukame 

WAKATI Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Jijini (DAWASA) ikiwahakikishia wakazi wa Jiji la Dar es Salaam juu ya kuwepo maji ya kutosha, wakazi wa maeneo ya Ubungo kwa muda wa mwezi sasa wamekumbwa na ukame mkubwa. 

Ukosefu mkubwa wa maji umejitokeza zaidi Ubungo Kibangu ambako wananchi wamekuwa wakihangaika huku na kule kusaka maji. 

Maji yaliyokuwa yakipatikana kwa mgao siku tatu kwa juma, hivi sasa hayapatikani tena ambapo wananchi hulazimika kutumiakj visima vilivyochimbwa baadhi ya maeneo. 

Mwandishi wa habari hizi aliwashuhudia akina mama kadhaa wakihangaika saa saba za usiku kutafuta maji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani. 

Baadhi ya wakazi wa eneo hilo wamelalamika kuwa huenda ukosefu huo wa maji unasababishwa kwa makusudi na baadhi ya wahusika. 

Wamedai kuwa hawaoni sababu ya msingi kwa eneo lao kukosa maji wakati wenzao wa maeneo ya Mabibo na Manzese hawana tatizo kama hilo ilhali bomba wanalotumia ni hilo hilo moja ambalo huingiza maji jijini toka mto Ruvu. 

Bwana Alawi mmoja wa wakazi wa eneo hilo alimdokeza mwandishi wa habari hizi kuwa bomba wanalotumia hilo ndilo hilo linalopeleka maji maeneo ya katikati ya jiji ambako hakuna shida hiyo. 

Aidha alisema wakati wao wako katika ukame, kiwanda cha pombe cha Kibuku kilichopo kando ya bara bara ya Morogoro kimeendelea kupika pombe kwa wingi kwa kutumia maji yanayosambazwa na bomba hilo. 



Waumini, Masheikh Arusha wasutana kwa futari ya Mrema 
 
  • Wahojiana uhalali wa futari hiyo
WAUMINI na Masheikh wao mjini Arusha wamekuwa katika tofauti baada ya kualikwa kula futari nyumbani kwa Mbunge Mh. Felix Mrema. 

Habari kutoka Arusha zimeeleza kwamba wiki iliyopita takriban Masheikh, wazee maarufu na Maustadhi wote mjini hapo walikusanyika kula chakula kilichoandaliwa na Bw. Felix Mrema kwa lengo la kuwafuturisha waungwana hao. 

Katika hali isiyo ya kawaida, inasemekana kwamba magari kadhaa yaliyokodiwa yalikuwa yakipita katika maeneo ya Misikiti kuwachukua waumini waliopata mwaliko. 

Baadhi ya waumini wamedai kuwa walihudhuria futari hiyo kwa kughilibiwa na Masheikh wao. 

Wamedai kwamba Masheikh hao waliwaambia kwamba Bw. Felix Mrema yu karibu kusilimu na hivyo kwenda kufuturu kwake ni kumpa nguvu. 

Waumini wamekuwa wakiwahoji Masheikh na Maustadh waliohudhuria futari hiyo kuelezea uhalali wa futari hiyo. Suala hilo limekuwa likiulizwa kwa kuzingatia kwamba muandaaji sio Muislamu. 

Baadhi ya waumini wamedai kwamba futari hiyo ni ishara ya kuanza kwa msimu wa tenda kwani 2000 inakaribia. 

Miongoni mwa Masheikh wenye heshima zao ambao walikataa kuhudhuria futari hiyo ni pamoja na Sheikh Mohamed Ahmad Anzuwan na Maustadh wa Msikiti wa Kijenge. 

Mialiko ya futari inakuja wiki moja tu baada ya gazeti moja la kidini kuripoti Sheikh aliyeshutumu tabia iliyoota mizizi miongoni mwa Waislamu ya kuhamanika na kula. 

Baadhi ya watu waliohojiwa na gazeti kuhusiana na hali hiyo, wamedai kuwa ni makosa kuwalaumu Masheikh kuitikia mialiko hiyo kwani ni kawaida kwa kumi la mwisho la mwezi wa Ramadhani kukirimiana. 

Hata hivyo, wamekuwa na wasiwasi na uhalali wa kuitikia mialiko ya wasio Waislamu na viongozi wa siasa. 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
Tahariri 
Baada ya futari nzuri: Tuwatupie macho wenye njaa 

Rais Mkapa kuwa mgeni rasmi Baraza la Idd 

Ubungo yakumbwa na ukame 

Waumini, Masheikh Arusha wasutana kwa futari ya Mrema 

Dondoo za saikolojia 
Na. Abu Halima Sa Changwa 

Waislamu turejee kwa Allah 

MSADAT yazidi kutia moyo Tanga 

Mjue Usama bin Ladin 

MAFUNZO KUHUSU FUNGA YA RAMADHANI 

Michezo isiyoruhusiwa katika Uislamu 

Ustadh Farid: Kijana aliyejitolea kuwapa Da'awa watalii 

Hakuna Magharibi wala Mashariki: Uislamu ni ubinaadamu 
Na Abubakari S. Marwillo 

Ijue madrasati Mar-wa ya Dodoma mjini 
Na Abu Zuberi, Dodoma 

Ijue Madrasat Jadidul Fiqhyyat - Tabata Kimanga 
Na B. Mwakangwale 

Madrasat Hidayatul Muumini Mwadui 

Washindi wa mashindano ya Hadithi za Mtume (s.a.w.) wapatikana 

Madrasa Shafii Ujiji Kigoma yaonyesha umahiri wake 

Waanzisha mifuko kusaidia wagonjwa Dodoma 

Waislamu Kondoa waomba msaada kumalizia Msikiti 

Mnyororo wa imani-2 
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa 

Kutoka magazeti ya zamani: 
Wanaoshitakiwa kwa uhaini kortini leo 

Jengo la Waislamu Moshi lageuzwa Kanisa la Walokole 
Na Mwandishi Wetu, Moshi 

Masjid Nurania yaswaliwa Ijumaa 
Na Rajab Rajab, Morogoro 

Jabal Hira kutoa mafunzo ya Kompyuta Morogoro 
Rajab Rajab na Mussa Ally, Morogoro 

Sayansi na Teknolojia 
[Internet ni nini?] 

Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Thamani ya mlo wa Uyoga] 
 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtz.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita