AN-NUUR 
Na.185 Shawwal 1419, Januari 29 - Februari 4 , 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Upinzani dhidi ya Serikali ya Kiislamu wakati wa Khalifa wa Tatu Uthman bin Affan

Malalamiko mengine yaliyotolewa na wanafiki wale ni kuswali swala kamili bila kupunguza katika Hija, kupiga mahema Minna na kutoza Zaka ngamia - mambo ambayo wakati wa mtume (s.a.w.) wala Abubakr na umar hayakufanywa. Kuhusu kutopunguza swala Khalifa alipoulizwa alisema nimefanya hivyo ili wakazi wa maeneo hayo wasidhanie kuwa kupunguza swala ndio utaratibu.80 Ama kuhusu mahema ni suala la maendeleo na kwa watu wa leo ni jambo halina msingi kabisa. Kwa vile mahema na nyumba za kitalii zinatumika sio Mna tu bali hata Makka. Ama kuhusu farasi kutozwa au kutotozwa Zaka wakati wa Mtume na makhalifa wawili wa mwanzo yaweza kuwa uchache wao na kushiriki kwao kwenye vita. Wakati wa Khalifa uthman na baada ya mfululizo wa vita hali ya uchumi ya Waarabu ilibadilika na Khalifa aliona ni Busara Zaka pia itolewe kwa farasi kama ilivyo kwa ngamia.81 

Sababu hasa ya chanzo cha ghasia hatimae kumuua Khalifa Uthman hazikuanza wakati wa uthman bali zilianza wakati wa Mtume (s.a.w.). Maadui wa Uislamu wakati wa Mtume walikuwa maqureish, Waarabu, Wayahudi, Wapersia na Wakristu wa Kirumi. Baada ya kutekwa Makka koo na makabila mengi yalisilimu, lakini walisilimu kwa nia mbali mbali ambapo hapa hatutazitaja. Linalothibitisha hili ni kule kuukana Uislamu kulikotokea mara baada ya kufa Mtume, uasi ambao uliikumba karibu Arabia yote. Wapinzani hawa walishindwa nguvu wakati wa Abubakr halikadhalika wakati wa Umar. Lakini haiyumkini kuwa walikuwa wameridhika na ustawi wa uislamu. Kwa hiyo hili ni kundi moja ambalo miongoni mwao walitokea wapinzani. 

Kundi la pili la wapinzani linatoka kwa wanafiki ambao njama yao ya kumuua Mtume ilitajwa kwenye Qur’an na hila zao kubainishwa mwaka wa 9 wa Hijria na hiki kilikuwa kipigo kikubwa kwao. Kubadilika kwa sera ya kuwataja wanafiki bayana na Mtume kukatazwa kuwaombea na kuwazika na kutotambulika katika jamii ya Waislamu kulistawisha chuki dhidi ya viongozi wa Waislamu. 

Kifo cha Mtume kiliwagawa Waislamu katika makundi matatu. Ukoo wa Mtume(Ahlul Bayt), Muhajirin na Answar. Pamoja na kuwekwa sawa hali hii wapo walioendeleza vikundi vyao moyoni na pale upinzani ulipochukua umbo la kuonyesha makosa serikalini. Bado lilikuwepo tatizo la mtu binafsi. Wapo Waislamu waliojiingiza katika upinzani kwa maslahi yao binafsi. Mfano mzuri ni Muhammad bin Abu Bakr na Muhammad Hudhaifa. 

Wayahudi nao hawakusahau kutolewa kwao Madina na hata huko Khaibar walikohamia bado walitozwa nguvu na kulazimika kulipa Jizya. Makundi yote haya yaliungana kwa kujuana na kutokujuana kwa kusimamisha upinzani dhidi ya Khalifa Uthman na serikali yake na hatimae kumuua. 

Fitna za Abdullah bin Saba 

Pamoja na makundi mengi haya, kiongozi wa udhia wote huu ni Myahudi aliyekuwa mkazi wa Yemen aliyejulikana kwa jina la Abdullah bin Saba. Saba hakuwa anataka Uislamu, na alipanga mpango wa kuudhuru Uislamu mbinu aliyotumia ni kuingia katika Uislamu na kuupiga vita Uislamu kutoka ndani. Kwa kutumia hali ya mazingira ya wakati ule alitunga na kuhubiri imani zisizokuwemo katika Uislamu ambazo ni kila Mtume aliacha "Wasi" (administrator) mtawala (mrithi wake katika ujumbe wake) na wasi wake alikuwa ndugu yake, kwa mfano Mtume Mussa alimfanya Haruna kuwa "Wasi" na Mtume wasi wake ni ndugu yake ali. Na ali alikuwa mtu pekee aliyehalali kupewa Ukhalifa. 

Saba alifikia kiwango cha kusema kuwa makhalifa watatu waliotangulia Abubakr, Umar na Uthman sio wa halali. Namna pekee ya kurekebisha mambo ni kumuondoa Khalifa Uthman madarakani: 

(i) Akafundisha kuwa ni ajabu kuamini kuwa Nabii Isa atakuja kutoka mbinguni ili afuate Uislamu na kuupigania dhidi ya maadui na kuamini kuwa Mtume Muhammad (s.a.w.) hatarudi. Saba aliamini na kufundisha kuwa Mtume Muhammad kuwa ni mbora kuliko Mtume Issa na kwa kuwa Yeye Muhammad ndie Mtume wa mwisho basi atarudi. 

(ii) Hali kadhalika alianza kutoa tafsiri potofu za aya za Qur’an ili kuhalalisha imani zake.82 

Kwa hiyo mbinu moja aliyoitumia ni kuhubiri imani ptofu hizo. ali alimtaka aache maskhara haya lakini hakukubali. Hivyo katika ukhalifa wake Ali alimchoma moto saba, 83 katika mpango wake huu sabaa alichagua maeneo yaliyokuwa imara kijeshi, Kufa, Basra, Syria na Misri kama vituo vya kueneza shughuli zake. 

Madina hakupata wafuasi, hivyo alikwenda Basra na kuendesha shughuli zake za upinzani dhidi ya Serikali. Gavana wa Basra Abdallah bin Amir alimwita na kumhoji kwa sababu hii Sabaa aliogopa akaondoka Basra na kuwacha wafuasi wake chini ya uwongozi wa Hakim Hublah adui wa Gavana. 

Kutoka Basra alikwenda kufa ambako alipata wafuasi wengi. Gavana, wa Kufa Sa’d bin Al As alimwita Saba na kumuonya juu ya udhalimu anaoufanyia Uislamu. Hatua hii ilimfanya ahame Kufa aende Damascus ambako hakufanikiwa lakini alimteua Ashtar kuwa naibu wake na kuacha maelekezo kuwa ujumbe wake uendelee chini chini na yeye akahamia Misri.‘ Ambako kwa kuwa Gavana wa Misri Abdallah bin Sarah alikuwa katika vita vya Warumi, Saba alipata muda wa kupandikiza fikra zake potofu akapata wafuasi wengi na kuweza kuwasiliana na vituo vyake vya kufa na Basra. Wafuasi wa uasi huu, walitumia mikakati mingi ya kujiimarisha walijionyesha kuwa ni wacha Mungu na kushawishi watu waunde malalamiko dhidi ya Maafisa wa Serikali, Magavana na Khalifa. Walitawanya barua za kuonyesha udhalimu wa serikali hali ni madai ya uzushi. Barua hizi zilitumwa kwa wafuasi wa Saba nao wakawa wanazisoma hadharani. Walionyesha kuwa Ali Talha na Zubair Maswahaba maarufu kwa wakati ule waliwaunga mkono84 ili kuunda taswira ya kuonyesha kuwa kweli serikali ina matatizo. 
 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
  

Tahari 
Kama hakuna haki watu watachukua sheria mkononi 

Kupokelewa kwa malalamiko ya Waislamu: Masheikh wasubiri ukweli wa Mkapa 

Afariki baada ya kutokwa damu nyingi: Yadaiwa hakuwa na sh. 4,000 

Nyumba ya Wakfu iliyoporwa yarejeshwa 

Kamanda Gewe atakiwa amkamate Daniel 

Sheikh awasambaratisha walevi Liwale 

Msikiti wavamiwa na kuvunjwa milango, madirisha 

Mjue Usama bin Ladin -2 

Msikiti wa Mwinyimkuu wafanya sensa 

Njaa hakuna, tunategemea kula silaha 

Parole kwa mbinde! 

Mabaraza yawatetee Waislamu - Sheikh Bafadhil 

Hali ya Uislamu Lukulunge, Kongwa inatisha 

Waislamu Kondoa waagizwa kuyatunza magazeti ya ANNUUR 

I.P.C yatakiwa kujitangaza 

Kutoka magazeti ya zamani 

Sabato ni ya Waisraeli, Mungu alikwishaiondoa 
Na Muhibu Said 

Waislamu wachoma moto nguruwe 

Tume ya kubadili Katiba Kenya: Waislamu kuwakilishwa 

Waislamu Msonge waomba wanusuriwe 

Sayansi na Teknolojia 
[PELEKA FAX NCHI ZA NG’AMBO BURE! – (2)] 

Masomo ya Kiislam 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na Lishe 
[Mwongozo wa mlo wa kila siku] 
 
 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtz.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita