AN-NUUR 
Na.188 Shawwal 1419, Februari 12 - 18 , 1999 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Tahariri
Tusirudishane nyuma
 

WALIPOULIWA Waislamu pale Mwembechai mengi yalisemwa na viongozi wa serikali kuhalalisha unyama na mauaji hayo. Wapo waliodai kadhia yote ile ilichochewa na Balozi za nje, wengine wakaja na kisingizio cha uchochezi wa vyama vya siasa, lakini wengine wakadai ni suala la wakorofi wachache wanaotaka kuvuruga amani ya nchi. 

Katika ujumla wake, propaganda zote hizo zililenga kupotosha ukweli kwamba kadhia yote ile ilikuwa uonevu na dhulma dhidi ya Waislamu. 

Lakini baada ya vumbi la propaganda kutulia ukweli umejidhihirisha. Waislamu wote washasema lile lilikuwa la Waislamu wote na ule ulikuwa udhalimu uliofanywa na vyombo vya dola dhidi yao. 

Hilo limesemwa na Waislamu wa Taasisi na madhehebu zote nchini. Sasa tusirudishane tena nyuma. 

Tunasema hivyo kwa sababu inaonekana juhudi zipo kutaka kuturudisha nyuma. Wakati Rais keshapokea risala ya malalamiko ya Waislamu kwa mikono miwili, wapo bado watu wanasimama na kutuletea unyeti katika madai ya Waislamu. 

Tunalosisitiza hapa ni kuwa huko tushatoka. Hakuna unyeti wala kughilibiana. 

Hapa kuna wananchi Watanzania Waislamu waliodhulumiwa na wanaondelea kudhulumiwa na vyombo vya dola. Ni haki ya wananchi hao kuwalalamikia viongozi wao. 

Hatua iliyofikiwa ni ya kukusanya ushahidi wa madai ili kumsaidia Rais katika hatua zake za kuyashughulikia. 

Sasa kama atasimama mtu kwenye jukwaa lake liwe la siasa, gazeti, Msikiti au Kanisa akawashutumu Waislamu basi huo ni ushahidi usiohitaj uchambuzi wa kisayansi. Haraka apelekewe Rais. 

Yapo madhila mengi ambayo hayajasemwa. Hayo yajumuishwe pamoja na yale ambayo yapo wazi na hayajibiki. 

Mfano suala la elimu halijibiwi kwa kusema kwamba wanawake na watoto wa wafugaji nao wapo nyuma. Maelezo hayo hayakani kuwepo kwa dhulma, zaidi yataonyesha kwamba wanaoonewa ni wengi. 

Yanapotolewa majibu ya visingizio kwa madai mazito kama haya, tafsiri yake ni moja tu; kwamba wanaolalamika wasubiri kuona dhulma zaidi. Hatudhani Waislamu wataendelea kulifumbia macho hilo. 

Wengine wanaotaka kupotosha ukweli ni waalimu wachache waliojitokeza kuzuia haki ya mabinti wa Kiislamu kuvaa Hijab. Hilo hatutarajii tena kuwemo katika risala za kina Alhaj Madabida. 

Kama Mwalimu anaona ni haki yake kufanya kazi na pengine anajihisi anayo haki zaidi ya wengine, basi ajue kuwa binti wa Kiislamu ni haki yake pia kupata elimu katika nchi yake na kwake kuvaa hijab ni haki yake zaidi. 

Waalimu hawa wanaoonyesha chuki dhidi ya hijab tunaishi nao mitaani na tunashirikiana nao katika maziko, harusi na hafla mbalimbali. Hatuoni hizo chuki zao huko mitaani tunapokutana. 

Sasa isije ikawa hawa wapo mashuleni kama mawakala wa madhalimu wenye nia mbaya ya kuendeleza dhulma kisha kuvuruga amani ya nchi yetu. 

Yawezekana mawazo hayo si yao, hivyo ni vyema kutizamwa kwa tahadhari wasije wakasababisha wazazi Waislamu wakajikusanya mashuleni kuleta zogo. 
 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 

Tahari 
Tusirudishane nyuma  

Mwaka mmoja wa mauaji ya Mwembechai: Waliouawa ni wanne 
Na Mwandishi wetu 

Waasisi wa TAA waibuka kupigania haki zilizoporwa 

Kuhujumiwa Waislamu kielimu: Mzazi adai mwanafunzi Adam Rashid kafelishwa 

Maoni yetu: Tuondoleeni wenye mikono ya damu 

MARADHI YA KISAIKOLOJIA: MULTIPARAPHILIASIS 

Askari wa Tume ya Jiji wapora mkaa 

Kuchangia Radio Kheri Broadcasting Station 

Yesu Kristo na Yohana Mbatizaji 
Na BERNARD B. MWENDA 

Wakereketwa CCM wawakosha wauaji wa Mwembechai 
Na Idd Kikong’ona, Morogoro 

Ufugaji holela wa nguruwe waikumba Dodoma 
Na Abu Zubeir, Dodoma 

Watembelea na kusaidia wagonjwa Arusha 

Mkuu wa wilaya awatimua Masheikh ofisini kwake 
Na Mwandishi Wetu, Morogoro 

Kutoka magazeti ya zamani 

Sayansi na Teknolojia  
[Windows: Mambo Mazuri ya Kuyajua]  

Masomo ya Kiislam  

Barua za Wasomaji  

Mashairi 

Chakula na Lishe  
[Kauli hii ya serikali itatumaliza Watanzania kwa njaa]  

Kumbukumbu ya mauaji Mwembechai  
[Maazimio ya Maimamu Dar] 
  
 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtz.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita