Malya apewa Ukatibu baada ya kuhujumu mali za Waislam
  WAKATI Katibu wa Bakwata mkoani Kilimanjaro Bw. Rashid Malya akisambaza barua Misikitini akipinga kwamba hajauza jengo la ukumbi wa Bakwata; ushahidi mpya umeibuka ukithibitisha madai hayo.

Taarifa toka ndani ya Manispaa ya Moshi zimethibitisha kwamba Bw. Malya ameliuza jengo hilo na tayari alishatia kibindoni shilingi milioni mbili (2,000,000).

Pamoja na hujuma hiyo

aliyofanya dhidi ya mali za Waislamu Kilimanjaro, Bw. Malya amezawadiwa Ukatibu wa Kamati ya muda ya utendaji ya Bakwata Taifa.

Taarifa za awali ambazo zilichapishwa na gazeti hili ziliarifu kwamba jengo hilo limeuzwa na sasa walokole wanalitumia kama sehemu ya kuimbia kwaya zao.

Januari 29, kupitia barua yake Na. BMK/BWZMK/19/13, Bw. Malya aliwaarifu Maimamu wa Misikiti yote ya Mkoa wa Kilimanjaro akisisitiza kwamba "Jengo hilo halijauzwa".

Katika barua hiyo Bw. Malya alidai kwamba habari za ANNUUR zilikuwa za "kupotosha na kufarakanisha Waislamu" na kuongeza kwamba: "Ukweli ni kuwa jengo hilo halijauzwa".

Idara ya Elimu Manispaa Moshi ambao ndio iliyouziwa jengo, Februari 19, 1999 ilitoa barua ikithibitisha kwamba ni kweli wameuziwa jengo hilo kwa gharama ya shilingi milioni sita (6,000,000).

Katika barua hiyo Na. KNM.18/2/009/164 kwa Katibu wa Bakwata Moshi Mjini, Afisa Elimu Manispaa ameeleza kwamba Bw. Malya alipokea hundi ya malipo ya awali ya shilingi milioni mbili Juni 9, 1998 na akazitoa Benki Juni 10, 1998. Namba ya hundi hiyo ni 002358696 iliyoandikwa na kusainiwa Juni 8, 1998.

Kwa mujibu wa makubaliano, Bw. Malya anatarajiwa kupokea shilingi milioni mbili (2,000,000) za awamu ya pili hivi karibuni.
 

Juu RUDI


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtz.org
 
An-nuur Home | Ukurasa wa Mwanzo | Islam Tanzania 
Links | Matoleo Yaliyopita | Sign our Guestbook