AN-NUUR
Gazeti la Kiislamu la kila wiki - Tanzania
Toleo la Internet

Baada ya Nzasa mtihani mwingine kwa Rais Mkapa:
 
Vikongwe, watoto, wagonjwa watupwa nje na Tume ya Jiji  
  • Hukumu ya mahakama yatupwa
  • Wahoji mwananchi hana haki? Uhuru uwapi?
Na Mwandishi Wetu  

RAIS Benjamin William Mkapa anakabiliwa na mtihani kuhusiana na malalamiko ya wananchi juu ya kudhulumiwa haki zao na kufanyiwa vitendo vya kinyama na mamlaka au vyombo vya Dola.  

Katika malalamiko ya hivi karibuni wananchi wa Yombo Vituka Lumo waliodai kuwakilisha familia 200 wamemlalamikia Mh. Rais kwamba wamebomolewa nyumba zao kinyume cha sheria na katika hali ya kudhalilishwa.  Endelea..

Kiswahili kitumike kuendesha kesi - Dk. Saffari
  • Asema kutumia Kiingereza ni kumnyima haki mshitakiwa
Na Mwandishi Wetu  

KUTUMIA lugha ya kigeni katika uendeshaji wa kesi mahakamani ni uvunjaji wa haki za binadamu.  

Hayo yamesemwa na mwanasheria Dk.Abdallah Saffari alipokuwa akihojiwa na mmoja wa wataalamu wa lugha ya Kiswahili nchini Bwana Mohammed Mwinyi juu ya muswada wa kitabu chake "Sheria ya Mashitaka na Utetezi".  

Dk. Saffari amesema wakati umefika kwa wanasheria nchini kuondokana na taasubi (ung’ang’anizi) kwamba Kiswahili hakijitoshelezi kuweza kutumika katika masuala ya sheria.  Endelea..

 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtz.org
 
An-nuur Home | Ukurasa wa Mwanzo | Islam Tanzania 
Links | Matoleo Yaliyopita | Sign our Guestbook
 
Gazeti hili huchapishwa na Islamic Propagation Centre, Box 55105, Dar es Salaam