Wako wapi Wajahidi? (Ushauri)
Niondoe mashakani, Mola uliye Jabali,
Unijaze yako shani, nipate kutawakari,
Fahari isiwe fani, nisije kutahayari,
Kikong’ona songa mbele, Mjahidi tawaona.
Uliko huko nyumbani, Kikong’ona zingatia,
Morogoro mlimani, jihadi wakumbushia,
Mjahidi watamani, akilini kuingia,
Kikong’ona songa mbele, Mjahidi tawaona.
Haki yako ya thamani, usikae kulalama,
Haki yako ithamini, uwe mfano nahoza,
Ukipita majumbani, vijana kuwaandaa,
Kikong’ona songa mbele, Mjahidi tawaona.
Watamka makusudi, jihadi kukumbushia,
Watokee mashahidi, haki kuipigania,
Haki ipate kurudi, dhulma kuiondoa,
Kikong’ona songa mbele, Wajahidi tawaona.
Kutokea mashahidi, yafaa maandalizi,
Kikong’ona ushahidi, hujitaji simulizi,
Kwa zile zako stadi, umepata ung’amuzi,
Kikong’ona songa mbele, Mjahidi tawaona.
Uwe nahodha jadidi, kufanya hii kazi,
Hutauliza shahidi, kwa hili jambo azizi,
Itashitadi jihadi, kwa ule wako ulinzi,
Kikong’ona songa mbele, Mjahidi tawaona.
Kusonga mbele sitaki, saba beti kituoni,
Kikong’ona uhaki, wasi wangu thamani,
Sitaki kukuzihaki, kwenye hii yako fani,
Kikong’ona songa mbele, Mjahidi tawaona.
Mlangano Mpunga Kawapa Wala,
Ubungo Islamic College of Education,
P.O. Box 55105,
DAR ES SALAAM
|
|