Na Mwandishi Wetu
WANAFUNZI wa shule ya Jangwani wamedai kuzuiwa kutumia chumba walichokuwa wamepewa kuswalia awali.
Kutokana na maelezo ya Mkuu wa Shule hiyo wanafunzi hao wamezuiwa kutumia chumba hicho baada ya yeye kupata habari kutoka Usalama wa Taifa kwamba upo mpango wa baadhi ya watu kujenga Msikiti shuleni hapo.
Awali wanafunzi hao walipewa chumba cha kuswalia ambapo waliamua kukifanyia ukarabati kwa vile kilikuwa na ubovu. Kabla ya zoezi hilo kufanyika Mkuu wa Shule aliwazuia wasikitumie.
Mwalimu Mkuu huyo Mama Theresia Mkamati amedai kuwa yeye aliendewa na watu wa Usalama wa Taifa wakidai kwamba panajengwa Msikiti shuleni hapo.
Kutokana na ujio huo inaonekana katika hali ya kujihami na kujitakasa ndipo hatua ya kuzuia sehemu ya majengo ya shule kufanyia ibada ikachukuliwa.
Juhudi za gazeti hili kuongea
na mwalimu huyo kwa njia ya simu hazikuweza kufanikiwa, hata hivyo mwalimu
wa dini shuleni hapo amethibitisha taarifa hizo, hata hivyo akadai kuwa
Mkuu huyowa shule hakutaka kutoa ufafanuzi wowote zaidi ya kusisitiza kuwa
alifikiwa na watu wa Usalama wa Taifa.
|
|