RAIS Yoweri Museveni wa Uganda amesema kwamba atakwenda Misikitini kuelezea ni kwanini serikali yake imeifunga Benki ya Greenland na kwamba hataifungua abadan.
Akihutubia Kamati ya Utendaji ya chama chake kinachotawala Uganda huko Jinja wiki iliyopita Rais Museveni amesema alipoamua Benki hiyo ifungwe baadhi ya watu wamedai kwamba kuna siasa.
Hivyo akasema kwamba ataitembelea
Misikiti nchini Uganda kutoa ufafanuzi . Hata hivyo Rais Museveni hakutoa
ufafanuzi nini maana ya kuwa na siasa katika jambo hili na kwanini awazungukie
Waislamu Misikitini kutoa ufafanuzi badala ya kuwaeleza wananchi wa Uganda
kwa ujumla. Endelea...
WATU kadhaa wasiokuwa Waislamu katika kijiji cha Mchito Dodoma Vijijini wameufuata na kuingia katika Uislamu imefahamika.
Akiongea na Mwandishi wa habari hizi katika ofisi za gezeti hili, Sheikh Salum Abubakar Kazi, alieleza kuwa yeye ni wa kwanza kusilimu kijijini kwao tangu mwaka 1991, baada ya kusilimu alipata mafunzo yake ya Uislamu Kimamba (Morogoro) kwa Sheikh Abubakar Swalehe Bombaheka kwa muda wa miaka mitatu (1993-95).
Baada ya kurejea nyumbani (Mchito) alikuta kuna Waislamu wawili, hivyo pamoja na yeye wakawa watatu; "Tulikuwa tukiendesha ibada zetu chini ya mwembe", alisema. Endelea...
|
|