AN-NUUR
Gazeti la Kiislamu la kila wiki - Tanzania
Toleo la Internet

Hali ya Uislamu Seregete Moro mbaya
Na Rajab Rajab, Morogoro

HALI ya Uislamu katika vijiji vya Seregete 'A' na 'B' vilivyoko katika kata ya Kidugalo, tarafa ya Ngerengere mkoani hapa ni mbaya kufuatia eneo hilo kutokuwa na walimu wa dini licha ya kuwepo Waislamu wengi.

Vijiji hivyo vilivyoko mwishoni mwa mkoa wa Morogoro na Pwani kupakana na kijiji cha Lukenge mkoa wa Pwani havina Msikiti wala madrasa ambapo Waislamu wanalazimika kufanyia ibada zao chini ya mwembe.

"Hapa ndipo tunaposwalia baadhi ya Waislamu wengi waliokuwepo hapa kijijini", alisema Bw. Abdallah Saidi Dakawa akionyesha kiwanja kilichofagiliwa chini ya mwembe huku kukiwa na mkeka mmoja pamoja na birika iliyoning'nizwa katika tawi la mti huo, mara baada ya kuulizwa na mwandishi wa habari hizi ni wapi sehemu wanapofanyia ibada zao. Endelea...
 

Kuweni macho na maadui - Mwinyi
 

Na Idd Katimba, Tabora

RAIS mstaafu Mh. Ali Hassan Mwinyi amewatahadharisha Waislamu wawe macho na wang'amue hatari iliyo mbele yao ambapo uadui na nguvu zote zilizo kuwa dhidi ya Ukomunisti zimeelekezwa katika Uislamu.

Amewaambia Waislamu kuwa kama ambavyo Ukomunisti umekufa; ni tamaa ya wapinzani wa Uislamu kuona nao unakufa au kusambaratika.

Alhaj Mwinyi aliyasema hayo akiwahutubia maelfu ya Waislamu waliohudhuria kuweka jiwe la msingi la Madrasa na Msikiti wa Mtendeni (TANESCO) eneo la Kiloleni. Endelea..

  


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtz.org
 
An-nuur Home | Ukurasa wa Mwanzo | Islam Tanzania 
Links | Matoleo Yaliyopita | Sign our Guestbook
 
Gazeti hili huchapishwa na Islamic Propagation Centre, Box 55105, Dar es Salaam