Na: Tahir Rashid
QUR'AN NI KITABU (2:2) na ni MUUJIZA ulio HAI - KISOMWI kilichotakaswa (98:2) Nuru ambayo kwayo (Allah) Humuongoza Amtakaye (42:52).
Ni agizo kwetu kuisoma (73:4) kwani ni ukumbusho kwa walimwengu wote (69:70) Hasa kwa yule anayetaka kushika njia (81:27-28) yakurejea kwa Mola wake (42:10).
Na Kitabu (hiki) hakikutemremshiwa (Mtume Muhammad) isipokuwa abainishie (watu) yale ambayo (1) Wanakhilitilafiana na (kiwe) (2) uongozi na (3) rehema kwa watu wanaoamini (16:64) ili Dini ihuishwe (16:65) kwa amri yake (na) watu waonyeke kuwa hakuna kiongozi ila Yeye (Allah), basi Aogopwe (16:2) Yeye tu. Yeye ndiye mwenye vyeo vya juu, Mwenyekiti (40:15) Kiongozi (wetu) mmoja tu (37:4), Rais wa mbingu na ardhi na yaliyomo kati yake; na ni Rais wa (nchi zote zilizoko) mashariki (na zilizoko Magharibi) (37:5).
Rais wetu huyu (Allah) Ametufanyia hisani kubwa waumini (vile) alivyomleta Mtume akatusomea Aya zake, na kututakasa na kutufundisha Kitabu na hikima (3:164), (ili tusalimike na) upotofu (huu tulionao sasa duniani) ulio dhahiri (3:164). Upotofu huu uliodhahiri ni kule kushika miungu mingine badala yake (36:23-24). Na miungu hiyo si wengine bali ni Viongozi bandia (wanaofarikiana 12:39) tuliowateka (15:96) na kuwapa vyeo (majina) tunavyopanga sisi wenyewe (12:40) pindi walipohitimu katika vyuo vikuu (9:31). Hivyo wao wanavyuoni wetu hawa na watawa (lao moja), wametuwekea dini (isiyokuwa ndiyo) (42:21) tulipowafanya sawa na Rais (Mola) wa walimwengu wote tulipowateua kuwa viongozi (26:98). Imekuaje tumegeuzwa (10:32) na kuingizwa kwenye upotofu kwa kumuweka Rais (Mola) wetu wa Kweli Allah? (10:31). Kiongozi anayeturuzuku kutoka mbinguni na katika ardhi, sio kutupeleka kuomba misaada kwa wazungu na kwa wachina 22:13) anayemiliki masikio na macho, amtoaye mzima katika mfu na kumtoa mfu katika mzima. Na hutengeneza mambo yote (10:31). Imekuwaje? Hatusadiki (10:31) hivyo tungojee kuthubutikiwa na kauli yake kwa kuasi kwetu? (10:33). La!
(Muhammad) alitumwa (kuja) kuongoza na (kutufunza) dini ya haki (chama cha kweli) ili aijaalie kushinda (kuchukua uongozi chama hiki) juu ya dini zote (vyama vyote); ijapokuwa watachukia MADEMOKRATI (WASHIRIKINA 30:31-32) (9:33). Kumbe neno washirikina limebatizwa na kuitwa mademokrati bila sisi kujua utaratibu wa maisha unajaalia watu kukhitilafiana.
IKHTILAFU:
Muhammad (47) kaletwa kubainisha Ikhtilafu iliyoko baina ya watu kwa wale wanaoamini (16:64) (wanaofuata aya za Allah 28:47).
Tujiulize ni nini Ikhtilafu? Jibu: Kwa wale wanaofuata Aya za Allah (28:47) Ikhtilafu ni ile Khabari Kubwa (78:2-3).
Kuwa macho ( ). Yaliyosemwa hapo ni kwamba, kwa wale waumini (28:47) wao Ikhtilafu ni ile Khabari Kubwa. Na nini basi kitakachokujulisha (90:12) hata akajua KHABARI KUBWA ni nini Jibu:
KHABARI KUBWA (38:67) ni yule mwingi wa Rehema, mwenye nguvu, Rais wa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake (38:66) Mmoja hakuna Kiongozi (Mungu) ila Yeye (38:65) Hivyo tuonyeke (25:1) kwamba Umma wetu huu ni Umma mmoja, na yeye (Allah) ni Rais wetu (21:92). (Lakini) jambo hili tumejiepusha nalo (38:68) na kulivunja baina yetu (tukafarikiana (21:93) na kuwa makundi makundi (30:53). Hivyo tumeshika miungu (viongozi) wengine badala Yake (42:9),
WITO WA MUHAMMAD
Mlinganiaji wa Allah akiita (46:31) "Enyi watu! Njooni katika neno lililosawa ....., ya kwamba:
1. Tusimuheshimu, wala kumuogopa wala kumuomba, wala kumpenda kupita kiasi [taz: Kamusi neno Abudu (kd)] yeyote yule ila Allah; wala tusimshirikishe na chochote (tusifuate matamanio ya nafsi 45:23); tusije wafanya wengine (wetu) kuwa viongozi badala ya Allah (nao ni wanavyuoni na watawa ambao tunawapigia kura) 3:64 kutomuitikia mlingani huyu (tukadai kuwa maongozi yetu haya, hayana dini); ndio kuwa katika upotofu uliodhahiri (46:32) Na jambo hili la kukataa uungu (Uongozi) wa Kiongozi mmoja ndio "Munkar" (16:22). "Munkari: uzuiliwe (ukataze (3:114), Eh!
Uongozi wa Allah ndio Uongozi (2:120) Kwa hiyo ikisemwa MUNKARI UZUILIWE, moja ya maana ni kwamba usiwepo Uongozi mwingine bighairi ya huu wa Allah. Jambo la leadership (uwongozi) ni wa nani; mtu asishindane nawe. Na walinganie watu kumwendea (kumwelekea kwa maongozi) Rais wako. Bila shaka wewe (Muhammad) uko juu ya uongozi ulio na msimamo (22:67-68). Mwenyezi Mungu anajua yote (wapinzani 38:2) wanayoyatenda (22:69), Hukumu ni Yake siku ya kiama katika Ikhtilafu (hii) (22:69) ya kumpa ukuu na ukubwa binadamu wenzetu tukawafuata (33:47) badala ya Allah ambaye ndiye Mkubwa na ndiye aliye juu, juu, juu, zaidi.(2:255).
(Itaendelea toleo lijalo)
|
|