AN-NUUR
Gazeti la Kiislamu la kila wiki - Tanzania
Toleo la Internet

Wanafunzi Waislamu wanyanyaswa Mkwawa
Na Mwandishi Wetu

TAARIFA ya TAMPRO tawi la Iringa imedai kwamba inaelekea uongozi wa shule ya Sekondari Mkwawa haifurahishwi kuwepo kwa wanafunzi Waislamu shuleni hapo.

Wanafunzi Waislamu ambao ni wachache sana shuleni hapo imedaiwa kwamba wamekuwa wakikerwa na kunyanyaswa na uongozi wa shule kwa tuhuma kwamba wanataka kuiharibu shule kwa Uislamu wao.

Imeelezwa kwamba wanachodai wanafunzi hao ni uhuru wao wa kuswali, kuvaa Hijab na majukumu mengine ya dini yao wakiwa shuleni. Endelea....
 

Serikali yashutumiwa kwa uvunjaji wa amani
Na Mwandishi Wetu

SERIKALI imeshutumiwa kuvuruga amani kwa vyombo vyake vya dola kuingilia masuala ya dini kinyume na Katiba na sheri za nchi.

Bw. Ndimbo ambaye ni Mkatoliki amemwambia Mkuu wa Wilaya ya Temeke kuwa serikali na vyombo vyake vinastahiki kubeba lawama zote za kuvunjika kwa amani nchini kwa vyombo vyake kuhusika kuanzisha vurugu katika mihadhara ya dini. Endelea...


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtz.org
 
An-nuur Home | Ukurasa wa Mwanzo | Islam Tanzania 
Links | Matoleo Yaliyopita | Sign our Guestbook
 
Gazeti hili huchapishwa na Islamic Propagation Centre, Box 55105, Dar es Salaam