Ubaguzi dhidi ya Waislamu Songea:
Masista wavaa vilemba vyao, Waislamu Hijaab marufuku
 

Na Mwandishi Wetu

JUMUIYA ya wanafunzi Waislamu mkoani Ruvuma wameelezea masikitiko yao juu ya ubaguzi unaofanywa dhidi ya wanafunzi Waislamu mashuleni.

Taarifa ya Jumuiya hiyo RUMUSA imedai kuwa wakati wanafunzi Waislamu wamepigwa marufuku kuvaa hijaab katika baadhi ya mashule wanafunzi watawa Wakikatoliki (masista) wanaosoma shuleni huvaa magauni yao na vilemba bila ya bughudha.

Aidha, imeelezwa kuwa katika shule ya sekondari ya wavulana ya Songea (Songea Boys) masomo yamekuwa yakiendelea wakati wa swala ya Ijumaa. Hali hizo huwafanya wanafunzi Waislamu ama wakose swala au vipindi.

Jumuiya ya RUMUSA inawajumuisha wanafunzi Waislamu wa shule za sekondari za Songea wavulana na Songea wasichana, Ruvuma sekondari, Ruhuwikopamoja na vyuo vya Ualimu Songea (TTC) na Afya (COTC).

Hivi karibuni RUMUSA iliandaa mahafali ya kuwaaga wanafunzi Waislamu wanaomaliza kidato cha sita katika mahafali hizo mgeni rasmi Bw. Abbasi Hussein kutoka CRDB aliwataka wahitimu kuitumia elimu yao vyema kutekeleza wajibu wao katika dini.

Baadhi ya Masheikh waliohudhuria sherehe hiyo walikuwa Sheikh Shaibu ambaye ni mshauri wa vijana wa Kiislamu mjini hapa, Sheikh Shaabani Mbaya ambaye amerejea hivi karibuni akitokea Makka katika ibada ya Hija, Sheikh na Imamu wa Msikiti wa Mkoa Masjid Hudaa Sheikh Mpaka, Imamu wa Msikiti wa Majengo, Sheikh Juma Sanga na Katibu wa Msikiti wa wilaya Masjid Nuru.

Wageni kutoka katika taasisi za dini ni uongozi wa AL-MALLID kanda ya Kusini ukiongozwa na Sheikh Mohammed Kawangu.

Pia Mwalimu wa kujitolea ambaye anasaidia kwa wanajumuiya wa sekondari kuwafundisha masomo ya ziada, Ustadh Yasini Mwaegamile ambaye pia ni mwanachama wa TAMPRO alihudhuria mahafali hiyo.

--

Juu RUDI


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtz.org
 
An-nuur Home | Ukurasa wa Mwanzo | Islam Tanzania 
Links | Matoleo Yaliyopita | Sign our Guestbook