Enzi Na. 1
Bure mnazuzuka, enzi ni kama
maua,
Hayakawi kunyauka, hili
ninachanganua,
Chini yakapukutika, mwisho
wake hivyo hua,
Enzi ni kama maua, hayakawi
kunyauka.
Maua hunawirika, vizuri yakachanua,
Lakini kubadilika, kupo
likawaka jua,
Mwisho yakaja toweka, kana
kwamba hayakua,
Enzi ni kama maua, hayakawi
kunyauka.
Msije kughafirika, kudhani
zake hatua,
Ni za kudumu miaka, sivyo
hivyo nachambua,
Mara hali hugeuka, yakesha
nafafanua,
Enzi ni kama maua, hayakawi
kunyauka.
Ole kwenye mamlaka, msije
kujifutua,
Enzi mliyoishika, yaweza
kujifungua,
Juu mkaporomoka, hadi chini
mkatua,
Enzi ni kama maua, hayakawi
kunyauka.
Mwembechai hekaheka, mambo
mmeyatibua,
Watu mlivyowafyeka, utadhania
mabua,
Bado Ponda mwamsaka, ni
mambo ya kushtua!
Enzi ni kama maua, hayakawi
kunyauka.
Itakuja kufutika, enzi mliyochukua,
Nyinyi zidini mahoka, tutakuja
washushua,
Mtu cho huanguka, kufumba
na kufumbua,
Enzi ni kama maua, hayakawi
kunyauka.
Mpanda ngazi hushuka, usemi
huu murua,
Kiingiacho hutoka, mzima
huja ugua,
Enzi huja huondoka, jueni
msiojua,
Enzi ni kama maua, hayakawi
kunyauka.
“Ni Mkonikoni wa Washairi”,
Abdallah Ahmad Seif (Ngoma
Imara),
S.L.P 1786,
Mtaa wa Airport - Dodoma
“Jimbo la Kati”.
Kuzaa na kuzaliwa (Kinyale)
Yeye wa tangu na tangu, mwanzo
mwisho Yeye hana
Mmoja Mwenyezi Mungu, katu
mshirika hana
Muumba nchi na Mbingu, na
vyote vilojazana
Kuzaa na kuzaliwa, Mwenyezi
kaepukana.
Mfanowe hana Mungu, kiumbe
akafanana,
Si watatu kwenye mbingu,
baba, roho, wala mwana,
Yangalizuka majungu, sheria
kufarakana,
Kuzaa na kuzaliwa, Mwenyezi
kaepukana.
Halali hachoki Mungu, hasahau
Subhana,
Mjuzi wa mambo chungu, yote
yalofichikana
Kwenye ardhi na mbingu,
hanaye wa kushindana,
Kuzaa na kuzaliwa, Mwenyezi
kaepukana.
Mlezi Mwenyezi Mungu, atulisha
Maulana
mtandazaji mawingu, mmvua
zanyesha mwanana,
Minanasi na mikungu, miembe
inashonana,
Kuzaa na kuzaliwa, Mwenyezi
kaepukana.
Kaumba Mwenyezi Mungu, Sura
kutofuatana,
China, Mwarabu, Mzungu,
rangi zisizofanana,
Kabila za ulimwengu, kilugha
zinapishana,
Kuzaa na kuzaliwa, Mwenyezi
kaepukana.
Razaku Mwenyezi Mungu, Mgawaji
kwa mapana,
Atupa pweza na changu, bahari
wazaliana,
Michuzi yajaza chungu, Samaki
wanoneana,
Kuzaa na kuzaliwa, Mwenyezi
kaepukana.
Muweza Mwenyezi Mungu, sifaze
ni nyingi sana,
Nemaze kwako na kwangu,
tele zimerundikana,
Kuhesabu kwa mafungu, idadi
yashindikana,
Kuzaa na kuzaliwa, Mwenyezi
kaepukana.
Beti nazifunga pingu, mwisho
ninatulizana,
Nawapisha na wezangu, sitaki
kusema sana,
Waseme sifa Mungu, wazame
wendo kwa kina’
Kuzaa na kuzaliwa, Mwenyezi
kaepukana.
Idd S. Kikong’ona
Morogoro
Tubadili Tabia
1.Bismillahi jalali, usopungukiwa
fani,
Mjuzi wa kila hali, umekosa
mpinzani,
Kwa mujibu wa Rasuli, Akhera
na duniani
Tuzibadili tabia, Ukimwi
Una hatari.
2. Ukimwi una hatari, nami
asoutambua,
Unaondoa kiburi, Mbishi
kuangamia,
Mwisho wake ni kaburi, shimoni
kukufukia,
Tuzibadili tabia, Ukimwi
una hatari.
3. Ukiukwaa jamani, sio kama
malaria,
Haitofaa (Quinini), (Fansidal)
nawambia,
Utazidi kuwa duni, muda
mrefu ugua,
Tuzibadili tabia, ukimwi
una hatari.
4.Tajiri na maskini, wote
ni sawa jamani,
Nafuu hawaioni, maradhi
ni namba wani,
Kwa pamoja ni sandani, Jenezani
kaburini,
Tuzibadili tabia, ukimwi
una hatari.
5. Dini kuishikamana, Salama
tutaipata,
Zinaa tukaachana, Ndoa hadhi
zikapata,
Kondom siyo maana, Vijidudu
vinapita,
Tuzibadili tabia, Ukimwi
una hatari.
6. Mwenye dini anatisha,
itikadi kuishika,
Ana msimamo tosha, kwa jambo
lenye mashaka,
Huwezi mshurutisha, mpira
ni uhakika,
Tuzibadili tabia, ukimwi
una hatari.
7. Bali dini atajali, zinaa
ataepuka,
Kukurubia muhali, kitabuni
imetoka,
Ataipitia mbali, Haitaweza
mfika,
Tuzibadili tabia, Ukimwi
una hatari.
8.Kwa herini nawaga, shikeni
wenye imani,
Nasema bila Uoga, siyomimi
Qur’ani,
Abishae kama boga, Hajawa
mtu jamani,
Tuzibadili tabia, Ukimwi
una hatari.
Said Khamisi Mkama
C/o Zuberi Mtemvu
P.O. Box 65
Sweet Cooner
Mtwara
Tuweni na Istiqama
Naanza kwa jina lake, Mola
Muumba dahari,
Hakika yeye yupweke, kwa
hili lilafakari,
Hakuna mfano wake, ila huu
mashuhuri,
Lazima tuwe wakweli, yapasa
Istiqama.
Pili natoa salamu, kwale
wangu wa linu,
NOLO aliye hitimu, na wengine
nifahamu,
NinakiRi muhamu, si kuwa
ime hasimu,
Lazima tuwe wakweli, yapasa
Istiqama.
Istiqama lazima, kama wewe
ni mkweli,
Akina baba na mama, lazima
tuyakubali,
Ni kauli ya Karima, siwe
na nafsi mbili!
Lazima Istiqama, kama wewe
Muumini.
Achana na unafiki, Muislamu
wewe vipi!
Mbona hutambuliki, biskuti
au pipi?
Kuku au mishikaki, bora
sema sasa kipi?
Achana na unafiki, lazima
Istikama.
Elfu mbili nafika, lazima
kuhamasisha,
Vibudu vilivyo chuka, achana
navyo si hasha,
Tafuta kisicho chuka, kilicho
ndani ya kasha,
Lazima tuwe wakweli, Istiqama
ni njema.
Lililopita sindwele, sasa
tungange lijalo,
Sio tupige kelele, tulishike
sasa hilo,
Hakuna tena sumile, chakua
ulitakalo,
Kama wewe umuumini, lazima
Istiqama.
Hapa na keti uchani, kwanza
nataka pumua,
Ilah Mola Manani, utupe
nyingi afyaa,
Na pia tupe afweni, kama
tumodhamiria,
Lazima tuwe wakweli, tuweni
na Istiqama.
Rashidi N. Moh’d (Mdabi)
S.L.P. 55105
Dar es Salaam
--
|
|