AFYA
 
Magonjwa ya kuambukiza -3
 

Homa ya uti wa mgongo (Meningitis)

HOMA ya uti wa mgongo ni miongoni mwa magonjwa hatari sana ambao huua haraka. Ugonjwa huu hushambulia ubongo na uti wa mgongo hasa kwa mwatoto.

Unaweza kuanza kama tatizo la ugonjwa mwingine kama vile surua, kifaduro au kukohoa. Watoto ambao wana kifua kikuu (TB) mara nyingine hupata TB ya ubongo na uti wa mgongo (tubevculosis meningitis) wakiwa na umri wa miezi michache tu.

Dalili: Ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo hutambulika kwa dalili zifuatazo. Homa, mkazo wa shingo, mgongo kupinda kwa nyuma. Kwa watot walio na umri chini ya mwaka mmoja utosi uvimba wakati mwingine degedege hutokea au kujitupatupa ovyo ovyo na hali inavyoendelea kuwa mbaya hupotewa na fahamu. TB ya ubongo huanza taratibu kwa muda wa siku au wiki. Aina nyingine zote za homa za uti wa mgongo huanza mapema zaidi kwa masaa au siku.

ili kukinga TB ya ubongo, watoto wote lazima wapate zindiko la BCB mara tu wanapozaliwa. Kwa kupande wa tiba inashauriwa mgonjwa apelekwe hospitali haraka.
 
--
Juu RUDI


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtz.org
 
An-nuur Home | Ukurasa wa Mwanzo | Islam Tanzania 
Links | Matoleo Yaliyopita | Sign our Guestbook