Na Mwandishi Wetu
CHAMA cha CCM kimetangaza kuanza rasmi kupambana na wapinzani wake katika medani ya siasa kwa njia za kihuni.
Aidha, Chama hicho kimedai kuwa wana CCM ndio wenye uwezo wa kuviamrisha vyombo vya dola vimuweke ndani nani
Aidha, Chama hicho kimedai kuwa wana CCM ndio wenye uwezo wa kuviamrisha vyombo vya dola vimuweke ndani nani na yupi vimwache. Kwa ajili hiyo kimewaagiza vijana wa CCM wawacharaze bakora wafuasi wa CUF na wale wenye ndevu ndefu.
Waislamu hasa wenye kufungamana barabara na suna ya Mtume (s.a.w.) juu ya ndevu na sharubu ndio wenye utambulisho wa ndevu ndefu.
Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni juzi huko Manzese, Katibu Mwenezi wa Chama hicho Wilaya ya Kinondoni Baraka Konisaga alisema kuwa ametumwa (na CCM) awaambie wana CCM kuwa wawashughulikie na wala wasiogope kwani serikali ipo chini yao; na kwamba watangaze rasmi kwamba sasa ustaarabu umeishinda CCM wanapambana kihuni.
Katika kutekeleza uhuni huo, Katibu huyo Mwenezi wa CCM ndipo amewaagiza wafuasi wa CCM wakiona watu wenye ndevu ndefu wawashughulikie.
Aidha, Katibu huyo alidai kuwa CCM ina taarifa kuwa wafuasi wa CUF watafanya fujo siku ya Ijumaa (leo) katika maeneo kadhaa Jijini.
Wananchi waliotoa maoni yao wamesema kuwa taarifa hii ya Katibu Mwenezi wa CCM ni nzuri kwani imetoa picha halisi ya mtizamo na mwelekeo wa chama hicho kwa wananchi wake.
Wamesema tatizo ni pale mtu anapojivika kilemba cha ukoka cha ustaarabu, udugu, uadilifu na malaika wa amani na utulivu asie na ubaguzi, lakini katika hali hii ya uwazi wananchi hawatatiziki.
Akitoa maoni yake baada ya mkutano huo, Bw. Saidi Omar wa Manzese alidai kuwa wananchi wapo kudai kile wanachoamini ni haki yao wanayoporwa na kwamba CCM inafanya kosa kubwa kunasibisha vuguvugu la wananchi na siasa za vyama.
Kwa kosa hilo alisema CCM kwa kutumia serikali yake yaweza kuidhibiti CUF na kuwacharaza bakora wote wenye ndevu, hata ikibidi kuwaua, lakini hiyo haitositisha wimbi la madai ya wananchi. "Wataendelea kusonga mbele hata wakiona wenzao wameuliwa", alisema Bw. Saidi.
Baadhi ya wachunguzi wa mambo
wamesema huenda taarifa hiyo imekusudia kujenga mazingira ya kuendesha
operesheni ya kukamatwa wafuasi wa CUF kabla ya siku ya uchaguzi ili kupunguza
idadi ya wapiga kura.
--
|
|