Kigwanda cha kijani!
Hasira zimenipanda, chini
sitaki kukaa,
Nachana changu kigwanda,
sikitaki kitambaa,
Moyoni nishakiponda, kibaya
kimefubaa,
“Chaa”, “chaa”, nakichana
chaa, kigwanda cha kijani.
Kimeukuwa cha kihuni, walevi
washinda baa,
Watu walo majununi, watendao
yasofaa,
Natupa sikitamani, Kiko
mwana wa Ulamaa,
“Chaa”, “chaa”, nakichana
chaa, kigwanda cha kijani.
Hamu kimeshanishinda, sinacho
tena tamaa,
Chanuka kama kidonda, che
funza wanozagaa,
No mana mwenye nakonda,
kimenijaza balaa,
“Chaa”, “chaa”, nakichana
chaa, kigwanda cha kijani.
Chake rihi ya Rwanda, damu
kimetapakaa,
Japo kimetoka Ndanda, nchini
sitakivaa,
Ndani ya changu kibanda,
sikipi tena wasaa,
“Chaa”, “chaa”, nakichana
chaa, kigwanda cha kijani.
Nikichome na motoni, kwa
mafuta yake taa,
Kitoke pangu machoni, kiwe
jivu la mkaa,
Linitoke la moyoni, dukuduku
lilojaa,
“Chaa”, “chaa”, nakichana
chaa, kigwanda cha kijani.
Nangoja hapo mwakani, rizuke
Jiji la Daa,
Nitafute madukani, chenye
rangi ya kung’aa,
Cheupe si cha kijani, kile
ninokikataa,
“Chaa”, “chaa”, nakichana
chaa, kigwanda cha kijani.
Mwisho mbele sitokwenda,
nakichana chana chanaa,
Bado niko njia panda, safari
naiandaa,
Wenzangu mnokipenda, oneni
yangu fatwaa,
“Chaa”, “chaa”, nakichana
chaa, kigwanda cha kijani.
Idd S. Kikong’ona,
Morogoro.
Mtu anayeropoka, hata zawadi
hapewi,
Umaarufu utang’oka, watu
hawakuelewi,
Na moto unaukoka, kuwaka
hauchelewi,
Hata zawadi hapewi, mtu
anayeropoka.
Matope anajipaka, amejenga
usodawi,
Tabia yake vilaka, ubora
haujengewi,
Halekebiki miaka, kwa ukweli
hauelewi,
Hata zawadi hapewi, mtu
anayeropoka.
Akili yake kichaka, ujinga
umesitawi,
Anazidi kujipaka, husikia
haelewi,
Amezoea kudaka, na kwa watu
haridhiwi,
Hata zawadi hapewi, mtu
anayeropoka.
Mwenye ameridhika, hajijui
hatakiwi,
Asemayo si hakika, hawezi
kufanikiwi,
Hapo alipo pashika, ukweli
haafikiwi,
Hata zawadi hapewi, mtu
anayeropoka.
Semanae ukacheka, kama mnyama
haliwi,
Ubaya umteka, na wala hajaribiwi,
Na pia kazoeleka, umwambia
aambiwi,
Hata zawadi hapewi, mtu
anayeropoka.
Wajuzi wanagutuka, haramu
hairudiwi,
Mipaka imeivuka, kila sehemu
ni tawi,
Ni vema ukaepuka, hasikikii
ni kiziwi,
Hata zawadi hapewi, mtu
anayeropoka.
Kaditama nimefika, yabidi
apigwe kiwi,
Amezidi kujipika, ajulikanavyo
ziwi,
Hawezi kuaminika, kwa umma
agombaniwi,
Hata zawadi hapewi, mtu
anayeropoka.
(Jua la usiku)
Ramadhani M. Nyembe (Siri
ya Nyumba),
S.L.P. 943,
Dodoma.
Ewe dada Islamu
Bismillahir naanza, kwa jina
lake Rabuka,
Tena kanipa uweza, kusoma
na kuandika,
Nia ni kuwaeleza, wasia
wangu hakika,
Acha kujidhalilisha, ewe
dada Islamu.
Islamu wa kisasa, kwa kweli
wanishangaza,
Waichukua mikasa, nakupita
itangaza,
Waicheza kwasa kwasa, njiani
bila kuwaza,
Acha kujidhalilisha, ewe
dada Islamu.
Amekuwa hayawani, hujuwi
kikudhurucho,
Kila onacho njiani, wakitaka
uwe nacho,
Yakushinde miwani, yakaapo
kwenye jicho,
Acha kujidhalilisha, ewe
dada Islamu.
Yarabi katuumbia, sura za
kila namna,
Sie twajiharibia, twajiweka
kwa namna,
Ngoziye kuikoboa, nazo nyuso
kuzichuna,
Acha kujidhalilisha, ewe
dada Islamu.
Hivi huna hata haya, kukataa
bara lako,
Vipi wale wa Ulaya, wakitaka
kuja kwako,
Wakimbilia Ulaya, na nywele
kama ukoko,
Acha kujidhalilisha, ewe
dada Islamu.
Mashindano uremboni, ndiyo
hayo mwayaweza,
Utakuta gazetini, uchi mmejilegeza,
Hata huko mashuleni, nao
pia wajikaza,
Acha kujidhalilisha, ewe
dada Islamu.
Acheni mfananisho, kati yako
na kondoo,
Yaja siku ya kitisho, ukate
ndugu na koo,
Kikutoke na kijasho, hiyo
siku ya kitisho,
Acha kujidhalilisha, ewe
dada Islamu.
Nane beti namaliza, kalamu
naweka chini,
Namshukuru muweza, kuniweka
akilini,
Kanijalia uweza, unifae
maishani,
Acha kujifananisha, kati
yako na wanyama.
Asha Juma,
Msamala Muslim Seminary
Sec. Sch.,
S.L.P. 985,
Songea.
|
|