Buriani Issa na Salala
1. Bisimilahir Rabani, Wahariri
nipokeeni,
Rambi rambi za Gongoni,
pia Tabora mjini,
Machozi mengi machoni, Ulamaa
kwaherini,
Buriani Sheikh wetu, Issa
pia Salala.
2.Sheikh Issa katutoka, Salala
amemfata,
Huzuni imetufika, msiba
ulotupata,
Machozi yalitutoka, habari
tulipopata,
Buriani Sheikh wetu, Issa
pia Salala.
3. Ni Ijumaa hakika, Sheikh
Issa katutoka,
Hakika umeitika, wito wake
Rabuka,
Machozi yatiririka, maSheikh
wametutoka,
Buriani Sheikh wetu, Issa
pia Salala.
4. Khatibu wa Ijumaa, kabla
hujaondoka,
Ulisalisha jamaa, usia ulikutoka,
Hapo ndipo ulikoma, hadi
ulipoondoka.
Buriani Sheikh wetu, Issa
pia Salala.
5. Mwembechai ni sababu,
kanda uliangalia,
Na kifo kikakusibu, dunia
ukakimbia,
Ukatutoka muhibu, ukaenda
kwa Jaalia,
Buriani Sheikh wetu, Issa
pia Salala.
6. Muda mfupi hakika, Salala
alipotutoka,
Salala alitutoka, mwezi
wa nne hakika,
Mji ulisisimka, machozi
yalitutoka,
Buriani Masheikh, kiama
tutaonana.
7. Hao ni Maswahiba, wa chanda
na kidole,
Tofauti kwao haba, wakarimu
na wapole,
Leo tena roho zakaba, Gongoni
nawapa pole,
Buriani Masheikh, kiama
tutaonana.
8. Salala kenda na presha,
pia Issa Imemsibu,
Hakika imetutisha, Tabora
nzima karibu,
Hakuna aliyebisha, Mola
ametujaribu,
Buriani Masheikh, kiama
tutaonana.
9. Kalamu naweka chini, majonzi
tele moyoni,
Alley nawausieni, mlobaki
subirini,
Kaburi zao ni jirani, wote
sisi tu njiani,
Buriani Masheikh, Issa pia
Salala.
Alley Mselem,
S.L.P. 935, Tabora.
--
--
|
|