Mirathi katika Uislamu - 3


KATIKA baadhi ya matoleo ya AN-NUUR miaka iliyopita tulieleza kwa kina falsafa ya mirathi katika Uislamu. Lakini suala al mirathi kwa mujibu wa sheria za Kiislamu limekuwa likiwakera sana wasioutakia mema Uislamu na miongoni mwao wamo wanaojiita Waislamu. Huenda ikawa suala hilo limekuwa likiibuka mwaka hata mwaka kwa sababu halijapatiwa ufumbuzi wa kudumu kwa Waislamu kuelimishwa juu ya haki zao katika Uislamu za kutaka sheria ya mirathi ya Kiislamu ibadilishwe kwa kuwa inambagua mwanamke. Kelele zinasikika kila mara jamii inapojadili sheria mbalimbali za mirathi na wanapoichambua sheria ya mirathi ya Kiislamu hufanya hivyo bila kufahamu msingi wa sheria yenyewe. Katika sehemu ya pili ya makala haya BI. HAWRA SHAMTE anaeleza mantiki ya sheria ya mirathi katika Uislamu.

Ufafanuzi wa Aya (4:11-12) za Mgawanyo wa mirathi.

Aya tulizozirejea (4:11-12) zimetaja kwa uwazi na kwa ukamilifu watu wenye kurithi na mafungu yanayorithiwa. Wenye kurithi kwa wanaume ni kumi na tano (15). Watu hao ni:

1. Mtoto mwanamume

2. Mtoto mwanamume wa mtoto mwanamume (mjukuu)

3. Baba

4. Baba wa kwa baba

5. Ndugu mwanamume wa kwa baba na mama

6. Ndugu mwanamume wa kwa baba tu

7. Ndugu mwanamume wa kwa mama tu.

8. Mtoto mwanamume wa kwa ndugu mwanamume wa kwa baba na mama

9. Mtoto mwanamume wa ndugu mwanamume wa kwa baba tu

10. Ami (baba ndogo) wa kwa baba na mama (ndugu yake baba).

11. Ami wa kwa baba tu

12. Mtoto mwanamume wa Ami wa kwa baba na mama

13. Kijana mwanamume wa ami wa kwa baba

14. Mume

15. Bwana mwenye kumwacha mtumwa huru.

Wenye kurithi katika wanawake ni kumi (10) wafuatao:

1. Binti (mtoto mwanamke)

2. Binti wa mtoto mwanamume (mjukuu)

3. Mama

4. Dada wa kwa baba na mama

5. Dada wa kwa baba

6. Dada wa kwa mama

7. Bibi mzaa baba

8. Bibi mzaa mama

9. mke

10. Bibi mwenye kuacha mtumwa huru.

Kuzuiliana

Tumeona kuwa wanaume wenye kurithi ni 15 na wanawake wanaorithi ni 10. Lakini wote hawa 25 wakikutana pamoja hawawezi kuruthi wote bali baadhi yao hawazuuilia wengine wasipate kitu au wasipate fungu kubwa. Katika kipengele hiki tutaonyesha wanazuiliwa na wasio zuiliwa.

1. Mtoto mwanamume hazuiliwi na mtu

2. Mjukuu huzuliwa na mtoto mwanamume na kila mtoto wa kiumbne aliyeko mbali huzuiliwa na aliyoko karibu na marehemu

3. Baba hazuiliwi na mtu

4. Babu wa upande wowote huzuiliwa na baba au babu wa karibu zaidi (k.m. baba yake baba humzuilia babu yake baba).

5. Ndugu wa kwa baba na mama huzuiliwa na mtoto mwanamume au mjukuu au baba.

6. Ndugu wa kwa baba huzuiliwa na ndugu wa kwa baba na mama; na kila amzuiliaye yeye (huyo ndugu wa na mama; na kila amzuiliaye yeye (huyo ndugu wa kwa baba na mama) vile vile huzuiliwa na dada wa kwa baba na mama akiwa pamoja na binti au binti wa mtoto wa kiumbe (mjukuu) au wote wawili.

7. Ndugu wa kwa mama huzuiliwa na mtoto au mtoto wa mtoto mwanamume au baba au babu.

8. Mume hazuiliwi na mtu wala

9. Mke hazuiliwi na mtu

10. Binti hazuiliwi

11. Mama hazuiliwi

12. Bibi huzuiliwa na mama.

Mafungu yenye Kurithiwa.

Mafungu ya uruthi yaliyotajwa katika Qur'an (4:11-12) ni haya sita yafuatayo:

1. Nusu (1/2)

2. Robo (1/4)

3. Thuluthi (1/3)

4. Thuluthi mbili (2/3)

5. Sudusi (1/6)

6. Thumuni (1/8).

Mwenye kupewa mafungu

Katika warithi kuna wenye kupata mafungu maalum katika hayo mafungu sita; na kuna wasiokuwa na mafungu maalum ambao hupata kilichobakia baada ya wenye mafungu kuchukua mafungo yao au hupata mali yote ikiwa hapana wenye mafungu. Wasio na mafungu huitwa ASABA.

Wenye mafungu maalum katika urithi ni watu kumi na mbili (12) wafuatao:

1. Baba

2. Babu

3. Binti

4. Binti wa mtoto mwanamume (mjukuu)

5. Ndugu wa kwa mama

6. Dada wa kwa baba na mama

7. Dada wa kwa baba

8. Dada wa kwa mama

9. Mama

10. Bibi

11. Mume

12. Mke.

Asaba - Warithi wasio na mafungu maalum.

Asaba ni warithi wasio wekewa fungu maalum na kustahiki kupata mali yote ikiwa hapana mwenye fungu au kupata kilicho bakia baada ya wenye mafungu kuchukua haki yao. Asaba wenyewe wako wa aina tatu:

(a) Asaba kwa nafsi yake

(b) Asaba wa pamoja na mtu mwingine

(c) Asaba kwa sababu ya mtu mwingine

(a) Asaba kwa nafsi yake ni wale wanaume tu ambao uhusiano wao na huyu marehemu haukuingiliwa namwanamke. Nao ni hawa wafuatao:

1. Mtoto mwanamume

2. Baba

3. Baba

4. Babu (baba yake baba)

5. Ndugu wa kwa baba na mama

6. Ndugu wa kwa baba

7. Mtoto mwanamume wa ndugu wa kwa baba na mama

8. Mtoto mwanamume wa ndugu wa kwa baba

9. Ami wa kwa baba na mama

10. Ami wa kwa baba

11. Mtoto mwanamume wa Ami wa kwa baba na mama

12. Mtoto mwanamume wa ami wa kwa baba

13. Bwana na bibi mwenye kumuacha mtumwa huru

14. Asaba wa mwenye kuacha huru mtumwa.

(b) Asaba wa pamoja na mtu mwingine ni hawa wafuatao:

1. Binti akiwa pamoja na kijana mwanamume

2. Binti wa mtoto wa kiume (mjukuu) akiwa pamoja na mtoto mwanamume wa mtoto mwanamume (mjukuu wakiume)

3. Dada wa kwa baba na mama akiwa pamoja na ndugu wa kwa baba na mama.

4. Dada wa kwa baba akiwa pamoja na ndugu wa kwa baba

5. Dada wa kwa baba na mama au wa kwa baba akiwa pamoja na babu.

(c) Ama Asaba kwa sababu ya mtu mwingine ni dada wa kwa baba na mama au wa kwa baba tu atakapokuwa pamoja na binti au binti wa mtoto wa kiume au wote wawili.

Musharakah - Kushirikiana Fungu

Ingawa Asaba wote utaratibu wao wa kurithi ni mmoja lakini nani kati yao mwenye haki zaidi ya kurithi pindi wakitokea pamoja itategemea na uzawa wa karibu na uwiano wa uhusiano wa maiti. Kwa mfano, uhusiano wa kwa baba na mama una nguvu zaidi kuliko uhusiano wa kwa baba tu, kwa hiyo, asaba wa kwa baba na mama ana haki ya kurithi kuliko asaba wa kwa baba tu.

Tumefahamu kwamba, asaba hana fungu, bali huchukua urithi wote kama hakuna mwenye fungu, au huchukua kilicho haki baada ya wenye mafungu kuchukua chao au hukosa kabisa kama hakuna kilichobakia au wakati mwingine asaba wenye daraja sawa na mwenye fungu, watashirikiana fungu hilo. Kwa mfano: Amekufa mtu akaacha mume, mama, ndugu wa kwa mama zaidi ya mmoja na ndugu wa kwa baba na mama.

Ugawaji wa Mirathi:

- Mume ana nusu (1/2) = 3/6

- Mama ana sudusi (1/6) = 1/6

- Ndugu wengine wa kwa mama wana thuluthi (1/3) = 2/6.

Hapo utaona kuwa mafungu yote sita yamegawiwa ya kaisha na ndugu wa kwa baba na mama hawakupata kitu. Hapa itabidi ile thuluthi waliyoipata ndugu wa kwa mama wagawane sawa sawa na ndugu wa kwa baba na mama maana nao wanayo haki ya ndugu wa kwa mama kama wao na wala hakoseshwi kwa sababu ya uasaba wake.

Kurithisha kwa kutumia mifano mbali mbali

Wakikutana warithi na pakawa hapana amzuiliaye mwenziwe na ikawa wote ni Asaba, wataigawanya mali iliyopo sawa sawa kwa kadri ya idadi yao. Kwa mfano, akifa mtu, akawa ameaacha vijana wanaume wanne, mali yote itagawanywa mafungu manne sawa sawa na kila mmoja apewe fungu lake.

Ama wakikutana asaba wanaume na wanawake, basi kila mwanamume atahesabiwa kuwa ni wanawake wawili, na mali itapigwa mafungu kila mwanamume mmoja apewe mafungu mawili na kila mwanamke apewe fungu moja. Kwa mfano, amekufa mtu akaacha watoto sita, wanne wanaume na wawili wanawake. Wanaume wanne watahesabiwa kuwa ni sawa na wanawake wanne. Kwa hiyho mali itagawanywa katika mafungu kumi yaliyo sawa sawa. Wanaume watapata mafungu mawili kila mmoja na wanawake watapata fungu moja moja.

Iwapo warithi ni mchanganyiko wa wenye mafungu maalum na asaba, itabidi kutafuta kigawe kidogo cha shirika (lowest common multiple (LCM) ili kupata mafungu yatakayhogawiwa kwa kila mrithi kwa kadri ya haki yake anayoistahiki. Hebu tuangalie mifano kadhaa ya mgawanyo wa mirathi.

Kwa mfano 1:

Amekufa mke na kuacha:

i) mume

ii) mtoto mwanamume

iii) baba

Wenye mafungu maalum kati ya hawa ni:

i) mume - ana robi (1/4) madhali yupo mtoto

ii) baba ana sudusi (1/6) madhali yupo mtoto.

Asaba Mtoto mwanamume na atachukua kitakacho bakia.

Ugawaji

Mafungu yatakayotolewa ni 1.4 na 1.6. Hesabu ndogo ambayo inaweza kutolewa mafungu ya urithi ni 12 yaani LCM ya 4 na 6. Kwa hiyo mali ya uryhtii itagawanywa kwenye mafungu 12 yaliyo sawa sawa na ugawaji utakuwa kama ifuatavyo:

i) Mume atapata 1/4 ya 12 (1/4 x 12) = 3

Yaani atachukua mafungu 3 katika mafungu 12 = (3/12 - 1/4)

ii) Baba atapata 1/3 ya 12 (1/6 x 12) = 2 yaani atachukua mafungu 2 kati ya mafungu 12 - (2/12 = 1/6).

iii) Mtoto atachukua mafungu yaliyobakia 12 - (3 + 2) = 7, yaani atachukua mafungu 7 kati ya mafungu 12 - (7/12)

Mfano wa 2:

Amekufa mume na kuacha wafuatao:

- mke mmoja

- mama

- mjukuu mmoja wa kike (binti wa mtoto mwanamume)

- mtoto mwanamume

- watoto watatu wanawake.

Kama mali iliyoachwa na marehemu ni Shs. 1,200/-, utarthisha wahusika kama ifuatavyo:

Ugawaji:

Wenye mafungu maalum kati ya hawa ni:

- Mke ambaye atapata thumuni (1/8) kwa sababu wapo watoto

- Mama atapata sudusi (1/6) ya mali kwa sababu wapo watoto.

Mjukuu hapati kitu kwa sababu wapo watoto ambao humzuilia

- Mtoto mwanamume na watoto wanawake watagawana mali iliyho bakia, wakiwa hao Asaba mwanamume achukue sawa na wanawake wawili (2:1).

Njia mbili zifuatazo zinaweza kutumika katika kurithisha wahusika:

(a) Hisabu ndogo inayoweza kutolewa mafungu ni 24. Yaani LCM ya 8 na 6. Kila fungu litakuwa na thamani ya Shs. 50 - (1,200 + 24). Kwa hiyo:

- Mke atapata 1/8 ya 24 (1/3 x 24) = 3 yaani atapata 3 x 50 = 150/=.

- Mama atapata 1.6 ya 24 (1/6 x 24) = yaani atapata mafungu 3 ambayo ni sawa na shs. (4 x 50) = 200/=.

- Asaba watarithi mali iliyobakia ambayo ni 1,200 - (150 + 200) = 850/-.

Mali hii itagawanywa katika mafungu 5 (kumbuka: mwanamume atapata sawa na wanawake wawili). Hivyo, kila mtoto wa kike, atapata Shs.1 x 850/- = 170/- na mtoto wa kiume, atapata Shs. 2 x 850 = 340/- .

(b) Njia ya pili ni kutafuta sehemu ya mali atakayoipata kila mwenye fungu maalum. Kama mali inayorithiwa ni Shs. 1,200/-.

- Mke atapata 1/8 ya 1,200/- = 1/8 x 1200 = 150/=

- Mama atapata 1/6 ya 1,200 = 1/6 x 1200 = 200/-.

Asaba watagawana mali iliyobakia ambayo ni 1200 - 350 = 850/-.

Kuna binti 3 na kijana mmoja ambaye ni sawa na binti 2. Hivyo mali iliyo bakia itagawanywa katika mafungu 5 ambapo kila binti atapata = Shs. 1 x 850 = 170/-.

na kila mama watapata sawa na binti 2 Shs. 2 x 850 = 340/-.

Kuongeza Mafungu (Awl)

Iwapo idadi ya mafungu yatakayogaiwa kwa warithi wenye mafungu maalum ni kubwa kuliko mafungu yaliyopatikana kwa njia ya LCM, idadi ya mafungu itabidi iongezeke ili kila mmoja apate haki yake.
--
JuuRUDI


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtz.org


An-nuur Home | Ukurasa wa Mwanzo | Islam Tanzania
Links | Matoleo Yaliyopita | Sign our Guestbook