TANGAZO

Bismillahir Rahmaanir Rahiim

ISLAMIC PROPAGATION CENTRE
TAMASHA LA AWAMU YA PILI YA UJENZI WA KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL
30 June - 14 July, 2000

Tunachukua fursa hii kuwatangazia Waislamu wote nchini kuwa tamasha la awamu ya pili ya ujenzi wa "Kirinjiko Islamic Secondary School" litaanza tarehe 30 Juni hadi 14 Julai 2000.

Awamu hii ya pili itahusika na kuinua majengo yafuatayo:-

(1) Mabweni 4
(2) Nyumba 5 za walimu
(3) Mabwalo 2 ya chakula
(4) Madarasa 4
(5) Msikiti

Waumini wote mnaombwa kushiriki katika tamasha hili kwa kuhudhuria au kwa kutoa mchango wa kuligharimia.

Watakao shiriki katika tamasha hili tunaomba wathibitishe kushiriki kwao na idadi ya siku watakazo shiriki kabla ya tarehe 25/6/2000.

Pia tunaomba washiriki waje na mchango wa chakula Tsh. 500/- kwa siku. Ambao hawatakuwa na uwezo wa kujigharimia chakula watuarifu kabla ya tarehe 25/6/2000.

Shime Waislamu! Tuimarishe mshikamano wetu na tuhudhurie kwa wingi.

Wabillahi Taufiiq
MKURUGENZI

--
JuuRUDI


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtz.org


An-nuur Home | Ukurasa wa Mwanzo | Islam Tanzania
Links | Matoleo Yaliyopita | Sign our Guestbook