Waafrika 400 wafa Angola
Mwafrika Julai 18, 1961
VITA vichafu viliibuka tena mjini Luanda katika Angola juzi ambako Wareno 14 waliuawa na 34 walijeruhiwa. Jumla ya waasi 400 wananchi wanaogombea uhuru wao wanasemekana wamekufa.
Majeshi ya Wareno yaliwazunguka maelfu ya wananchi na kuwaua wengi. Huko Quicabo, wananchi waliolipiza kisasi, wapatao 1000 walivishambulia vikosi kadha wa kadha vya Wareno kwa muda wa masaa 6 mfululizo, lakini walishindwa nguvu majeshi mapya ya Wareno yalipoletwa ili kuwaongeza wenzao nguvu kwa hiyo wananchi wengi waliuawa na silaha nyingi zao zilitekwa.
Majeshi ya Wareno kutokuwaua wananchi kwa haraka ili nchi itulie kunawakasilisha sana masetla na kuilaumu serikali. Wanalalamika kwamba mashamba 91 yameunguzwa moto na wananchi na mali nyingine kuibiwa. Pia wamesema kuwa mpaka leo wananchi wangali mabwana katika vita hivi na kwamba ustaarabu walioujenga kwa muda wa miaka mingi unaharibiwa bure na wananchi.
Mateso yatangazwa
Mateso wanayofanyiwa wananchi hayatangazwi kamwe na serikali katika magazeti au redio, lakini maneno ya dhiaka ya kuwatia more askari wa Kireno huchapwa, kama vile "Je, wakuu wa serikari na askari wa vita wamekwenda livu"?
Ni sehemu ya kaskazini ya Angola kuliko na mapigano makali, lakini kusini kuna afueni.
Sikio Oktoba 15, 1962
UGANDA iliingia katika jamii ya mataifa yaliyo huru ya ulimwengu mnamo usiku wa manane Oktoba tarehe 8, baada ya sherehe iliyovutia zaidi huko Kololo Kampala, ambayo ilikaa kwa muda wa masaa matatu. Punde baada ya ya bendera mpya yenye rangi nyeusi, manjano na nyekundu ilipokwisha kuinuliwa umati wa watu ulishikwa na kichaa kwa furaha na kwa muda wa dakika 20 baada ya usiku wa manane, waliona michezo ya marangi mengi yakifyatuliwa kwa viberiti vya michezo ya moto. Hii ilikuwa ishara ya kuwasha moto kila mahali juu ya vilima kokote nchini na kuanzisha maandalio na sherehe, ambavyo viliendelea hadi kulipokucha.
Mapema jioni hiyo, tuliona mchezo mkubwa uliopata kufanyika nchini Uganda.
ambamo karibu watu 1000 wa mataifa yote walishiriki. Hii ilikuwa tamasha kwa ajili ya uhuru wa Uganda ambamo mambo mengi yalionekana yakiwa kama vile muziki, kujinyoshanyosha miili, marangi na hata pamoja na makelele ya nguvu. Tukio lililokuwa lenye kelele nyingi zaidi ya yote kulikuwa kule kufyatuka kwa mizinga wakati makombora sita ya Royal Horse Artillery yalipofyatuliwa.
Sikio Oktoba 15, 1962
UGANDA iliingia katika jamii ya mataifa yaliyo huru ya ulimwengu mnamo usiku wa manane Oktoba tarehe 8, baada ya sherehe iliyovutia zaidi huko Kololo Kampala, ambayo ilikaa kwa muda wa masaa matatu. Punde baada ya ya bendera mpya yenye rangi nyeusi, manjano na nyekundu ilipokwisha kuinuliwa umati wa watu ulishikwa na kichaa kwa furaha na kwa muda wa dakika 20 baada ya usiku wa manane, waliona michezo ya marangi mengi yakifyatuliwa kwa viberiti vya michezo ya moto. Hii ilikuwa ishara ya kuwasha moto kila mahali juu ya vilima kokote nchini na kuanzisha maandalio na sherehe, ambavyo viliendelea hadi kulipokucha.
Mapema jioni hiyo, tuliona mchezo mkubwa uliopata kufanyika nchini Uganda.
ambamo karibu watu 1000 wa mataifa yote walishiriki. Hii ilikuwa tamasha kwa ajili ya uhuru wa Uganda ambamo mambo mengi yalionekana yakiwa kama vile muziki, kujinyoshanyosha miili, marangi na hata pamoja na makelele ya nguvu. Tukio lililokuwa lenye kelele nyingi zaidi ya yote kulikuwa kule kufyatuka kwa mizinga wakati makombora sita ya Royal Horse Artillery yalipofyatuliwa.
|
Links | Matoleo Yaliyopita | Sign our Guestbook |