Ndugu Mhariri
Naomba nafasi nitoe machache kuhusu uchaguzi wa Oktoba 29, 20000 kwa Waislamu.
Waislamu lazima tuelewe ili tusijekupata laana ya Mwenyezi Mungu. Sisi Waislamu hatupigi kura ili kumpata kiongozi atakayesimamia sheria za Kiislamu.
Bali Waislamu wote nchini tupige kura kama mkataba wa kupatiwa haki sawa kwa watu wote. Asiyetaka haki aelimishwe.
Ally R. Mpendu,
Keko - Mwanga,
Dar es Salaam.
Ndugu Mhariri
NAOMBA nafasi katika gazeti lako tukufu la AN-NUUR ili kutoa maoni yangu.
Ningewaomba wale Waislamu wanaolisoma gazeti hili kusoma kisa cha Bilal alivyokuwa akiteshwa na makafiri kumtaka akubali masharti ya hao makafiri. Sasa Waislamu Chama cha CCM mambo inayoyafanya ni sawa na kisa hiki, kwa sababu kinalazimisha watu kukikubali uongozi wao kwa hiyo Muislamu kukubali uongozi wa CCM itakuwa amekuunga mkono mambo haya yafuatayo:
Itakuwa umeunga mkono unyanyasaji wanaofanyiwa Waislamu hapa nchini.
Utakuwa umekubali mauaji ya Waislamu yaliyofanyika Msikiti wa Mwembechai.
Utakuwa umekubali kuwa kwa Muislamu Tanzania si lolote si chochote.
Kwa maoni yangu binafsi naiusia nafsi yangu na kuwausia Waislamu wenzangu kuyaangalia haya na dawa yake ni kutokuchagua CCM.
Mashaka Bamila,
Turiani,
Morogoro.
|
Links | Matoleo Yaliyopita | Sign our Guestbook |